PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: KWA NINI MASKINI WANAENDELEA KUWA MASKINI NA MATAJIRI WANAENDELEA KUWA MATAJIRI?
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
NA ANDREA NGOBOLE, PMT Swali moja kubwa linalowasumbua wanasosholojia na wataalam wa uchumi ni kwa nini maskini wanaendelea kuwa...


https://scontent.fjnb2-1.fna.fbcdn.net/v/t1.0-9/15941125_1270380289720137_5143866078369843999_n.jpg?_nc_eui2=v1%3AAeG1jAEuzLY7-7LfRdvl7CW4CBOQPGf6yL5N3HGMif8FfE-1trtuAYotJ3C3VGwf_FgULsAuRY2O8DFMb7rO2Jx4VGqt86veKtiwEuz0tKc5rrUOfz2EiseGPZeQYe3gqBI&oh=2fb256ff23f46e0facf4dc22f2d63f7d&oe=58D5C5A8

NA ANDREA NGOBOLE, PMT
Swali moja kubwa linalowasumbua wanasosholojia na wataalam wa uchumi ni kwa nini maskini wanaendelea kuwa maskini na matajiri wanaendelea kuwa matajiri vizazi na vizazi vyao vyote?

Swali hili ni gumu kidogo kulipatia jibu makini kama utafikiria kwa uchache ila ukweli ni kwamba umaskini na utajiri wote unatokana na fikra zilizopo mwa mhusika mwenyewe wa namna ya kuweza kuwa tajiri na au kuendelea kuwa maskini katika maisha yake na vizazi vyake vyote.

Kutokana na fikra hizo zilizojengeka akilini mwake na hujikuta mtoto wake naye hurithi fikra hizo kwa sababu ya jinsi anavyoongea naye, unakuta mzazi anakaa na mwanaye hukiri umaskini wake na kuona kama wao na uzazi wao walizaliwa ili wawe maskini kitu ambacho mimi binafsi sikubaliani nacho hata kidogo kwa sababu ambazo nitaziainisha baadae kidogo katika Makala hii.
Baada ya wanasosholojia kukaa na kufikiria sana juu ya namana ya kuweza kukomboa jamii maskini walijiuliza maswali haya yafuatayo




Maswali haya na mengine mengi yaliwalazimu kufanya utafiti wa sayansi ya jamii huko bara asia ili waje na majibu sahihi ya sababu haswa zinazofanya jamii maskini kuwa maskini

Waliamua kumtafuta mtu maskini kabisa asiyekuwa na kitu wakawa wanamfuatilia maisha yake kwa siku kadhaa wakaona kuwa ni  maskini na maisha yake ni ya chini sana wakamtegeshea mfuko wenye pesa nyingi sana kama milioni mia hivi za kitanzania na wakahakikisha yeye ndio anaziokota pesa zile basi wakaanza kumfuatilia wajue atafanyia nini hizo pesa?

Maskini huyo alipookota hizo pesa alifanya yafuataayo








Baada ya miezi miwili pesa zote zikawa zimeisha na kurejea katika maisha yake ya awali ya umaskini mkubwa usioelezeka tena Zaidi ya awali alivyokuwa

 Baada ya kupata majibu hayo watafiti hao wakaja na jibu moja kubwa na kusema sababu inayowafanya maskini kuendelea kuwa maskini ni kutokuwa na mawazo mazuri yatakayowaingizia pesa za kila siku

Wakashauri pia kila mwananchi afundishwe utawala wa fedha na mbinu za ujasiriamali ndio maana kwa sasa bara la asia ni moja ya mabara yanayokuja juu sana klatika kujikwamua kiuchumi ngazi ya familia na taifa kwa ujumla ndio maaana wahindi ni moja ya jamii toka barani Asia iliyosambaa dunia nzima wakijihusisha na biashara mfano kwa hapa Tanzania wapo wengi na wanaongoza kwa biashara pengine kuliko sisi wazawa ukienda mataifa ya marekani, Canada na uingereza kote huko utawakuta wanafanya biashara na wameushikiilia uchumi wa mataifa hayo.

Sasa ili uweze kuepukana na umaskini wa kipato lazima ukubali pia kubadilika kifikra na kiuchumi lazima uwe na nidhamu ya kutumia pesa yako kulingana na kipato chako yaani usitumie Zaidi ya unachokipata, lazima uepuke vitu vya anasa, lazima ujiweke lengo la kuwa tajiri na sio kuonekana tajiri, lazima uepuke starehe zisizo kuwa za lazima, lazima upende kujifunza mbinu za ujasiriamali toka kwa wafanyabiashara waliofanikiwa pia ukipata nafasi hudhuria semina za ujasiriamali ujifunze Zaidi lakini pia kutengeneza mtandao na watu waliofanikiwa

Matajiri wengi wanapenda kurithisha watoto wao utajiri na  huwafundisha mbinu za jinsi ya kuwa na kuendelea kuwa tajiri, huwaelekeza namna ya kuwa na nidhamu ya pesa, huwafunza matumizi ya pesa katika mgawanyo wa asilimia ambao nilishaueleza katika Makala iliyopita ya FANYA KAZI KWA BIDII ILI UUKIMBIE UMASKINI, huwapa mbinu mbalimbali za kubuni mali zalishi, huwapeleka katika vikao mbalimbali vya kibiashara wanavyokutana na wafanyabiashara wengine ili kuwazoeza namna kufanya biashara mbalimbali na hii ndio sababu ya matajiri huendelea kuwa matajiri.

Sasa naomba nikushirikishe jambo moja nalo ni Ili uweze kuwa tajiri unatakiwa uwe unajiuliza swali hili JE NIFANYE NINI ILI NIWEZE KUBADILISHA NA WATU KWA PESA ZAO?
Kwa sababu ulimwengu huu tunaoishi ni wa mbadilishano yaani kuanzia unachotumia kuanzia asubuhi mpaka jioni umetumia pesa ndio maana ukaweza kumudu kuvitumia kuanzia mswaki, dawa ya mswaki, ngo unazovaa, chai unayokunywa na kitafunwa chake usafiri unaokupeleka kazini na kurejea nyumbani vyote hivi umebadilishana kwa pesa. Kwa hiyo pesa zote ulizonazo sio zako kwa sababu zinaenda kununua mahitaji yako ya siku nzima usijali Siku nyingine Mungu akitujaalia nitakushirikisha namna ya kufanya pesa zako kuwa zako

Pia ili uweze kuwa tajiri lazima ujue maana ya mali na aina za mali
Mali ni kitu chochote chenye thamani iwe kubwa au ndogo ulichonacho kwa mfano simu, nyumba, gari, seti ya tv, radio,nguo za bei ghali kama suti, kuwa na kiwanja, sasa mali hizi zinakupa faraja ya kihisia tu kwamba nawe ni tajiri kwa kuwa unazo lakini ukweli ni kwamba kama hazikuiingizii chochote  wewe sio tajiri kwa sababu huingizi chochote kutokana na mali hizo

Pia kuna Aina za mali nazo  ni mali matumizi na mali zalishi ambapo mali matumizi ni zile mali zinazotumia kipato chako kila siku mfano ukiwa na gari  linahitaji mafuta ili liweze kutembea, unatakiwa ulipie road licence, bima na ufanyie service kila mwezi lakini halikuingizii chochote katika kipato chako cha siku ingawa inakurahisihia shughuli zako na mali zalishi ni zile mali ambazo zinakuingizia pesa kila siku mfano kuwa na nyumba ya kupangisha  wageni yaani guest house, kibanda cha kupigishia simu na au kuonesha mpira wa miguu na filamu, bajai unayoikodisha kwa ajili ya usafiri na kadhalika hizi ndio mali zalishi kwa sababu zinakuingizia kipato kila siku sasa hapa katika mali zalishi pia ujue kasi yake ya kukuingizia kipato  ni ipi mfano mwenye nyumba ya kupangisha anapata pesa kwa mwezi kwa hiyo kasi yake ya kuingiza pesa ni ndogo ukilinginisha mwenye nyumba anyefanya biashara ya kupangishia wageni kwa siku yeye huingiza pesa kila siku na hivyo kasi yake ya kuingiza pesa ni kubwa kuliko yule mwenye nyumba ya kupangisha anayesubiri mpaka mwezi uishe ndio apate kipato chake.

Ukishafahamu mali, mali matumizi na mali zalishi utaweka vipaumbele ni aina gani ya mali utanunua ili iweze kukukomboa toka katika lindi la umaskini  anza kujaribu kufikiria kuwa na mali zalishi nyingi Zaidi kuliko mali matumizi wataalamu wa uchumi wanaamini kuwa ili uweze kufanikiwa kiuchumi unatakiwa uwe na mali zalishi zisizopungua saba ndio unaweza kukaa na kusema sasa unaelekea katika ulimwengu wa mafanikio.

Ukiamua kubadilika kifikra utakuwa ni mmoja wa watu wataakaofanikiwa Zaidi kiuchumi na utapunguza kundi la watu maskini duniani na kuingia katika kundi la matajiri na kurithisha vizazi vyako vyote kuwa matajiri kwa kuwarithisha mbinu na maarifa ya jinsi ya kujikwamua kiuchumi wataalamu wa sosholojia wanaitaa hii ni social mobility yaani ni jinsi ya kutoka jamii moja kwenda jamii nyimngine mfano kutoka umaskini kwenda utajiri ni kazi ngumu sana lakinii inawezekana jaribu utaona

ASANTE KWA KUSOMA MAKALA HII UKIWA NA SWALI, MAONI AU USHAURI USISITE KUWASILIANA NAMI

NGOBOLE, Andrea Ashery.
0755780131
facebook.com/ Andrea Ngobole
facebook page, instergram na twiter ni  princemediatz

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top