Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akitembelea Mradi wa umwagiliaji katika kijiji cha Jobag wilaya ya Karau ,mradi uliojengwa kwa ufadhili wa shirika la Worl Vision |
Home
»
yanayojiri ARUSHA
» WAZIRI MKUU AZINDUA MRADI WA UMWAGILIAJI KARATU UTAKAOSAIDIA WAKULIMA 4000
Na Ferdinand Shayo,Arusha.
Waziri Mkuu
wa Tanzania Kassim Majaliwa amezindua mradi wa Umwagiliaji katika kijiji cha
Jobag wilaya ya Karatu uliofadhiliwa na Shirika la Worlvision ambao unahudumia
ekari 1200 na kuwafikia wakulima 4000.
Akizungumza
katika uzinduzi wa Mradi huo ,Majaliwa amesema kuwa mradi huo utasaida
kuchochea kilimo cha umwagiliaji hasa katika kipindi hiki ambacho kuna
mabadiliko ya tabia ya nchio na uhaba wa mvua.
Majaliwa
amesema kuwa Asilimia 80% ya Watanzania wamejiajiri katika sekta ya kilimo
idadi ambayo ni kubwa hivyo kilimo cha umwagiliaji kikihamasishwa ipasavyo
wakulima watapata tija kubwa na kuinua pato la taifa.
Aidha
amelishukuru shirika la Word vision kwa kujitoa kusaidia jamii katika eneo hilo
muhimu la kilimo ambalo ni tegemeo kwa wakulima wengi.
Waziri Mkuu
ameonya tabia ya baadhi ya watu wanaohujumu vyanzo vya maji kwa kuunganisha
mashine katika vyanzo na kufanya uharibifu hivyo amewataka kuondoka mara moja
katika chanzo hicho na iwapo watakaidi serikali itawachukulia hatua kali.
Mkurugenzi
wa Miradi katika shirika la World Vision Revocatus Kamara amesema kuwa mradi
huo utawanufaisha wakulima wengi na kupelekea upatikanaji wa chakula pamoja na
kukuza kipato cha wakulima.
Kamara
amesema kuwa shirika hilo litaendelea kushirikiana vyema na serikali ili
kufanya miradi itakayosaidia kutatua changamoto zinazoikabili jamii.
About Author

Advertisement

Related Posts
- FRIEDKIN CONSERVATION FUND WATOA MILLIONI 84 KUSAIDIA MIRADI YA MAENDELEO KWA JAMII YA MOYOWOSI, UVINZA NA UGALA02 Oct 20180
Baadhi ya wakurugenzi na viongozi wa Friedkin Conservation Fund wakiwa katika maonesho ya na...Read more »
- MOBISOL YASHIRIKI SIKU YA USAFI WA MAZINGIRA DUNIANI, WAHIMIZA MATUMIZI YA NISHATI JUA KUTUNZA MAZINGIRA17 Sep 20180
Baadhi ya wafanyakazi wa Mobisol Wakifanya usafi wa mazingira jijini Arusha mapema leo Baadhi ...Read more »
- JERRY MURRO ATOA MKWARA MZITO KWA WANAARUMERU MARA BAADA YA KUAPISHWA31 Jul 20180
Mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo katikati akiwa na wakuu wapya wa wilaya za Arumeru Bwana J...Read more »
- WAANDISHI WAWASILI KWA MGANGA WA JADI ILI KUMUELIMISHA JUU YA MADHARA YA UKEKETAJI KWA WATOTO WA KIKE.01 Jun 20180
Waandishi wa redio jamii tano Tanzania toka katika mikoa minne ya Arusha,Manyara,Dodoma na ...Read more »
- WAMAASAI, WASONJO WATAKIWA KUACHA UKEKETAJI01 Jun 20180
Jamii za Kimaasai na Sonjo zinazopatikana katika wilaya ya Ng...Read more »
- WADAU WA UTALII JIJINI ARUSHA WATOA MSAADA KUBORESHA HUDUMA YA AFYA31 May 20180
WADAU wa utalii mkoani Arusha wamekabidhi msaada wa Vitanda 40 kumi &nbs...Read more »
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.