PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: JERRY MURRO ATOA MKWARA MZITO KWA WANAARUMERU MARA BAADA YA KUAPISHWA
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
Mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo katikati akiwa na wakuu wapya wa wilaya za Arumeru Bwana Jerry Muro kushoto na kulia ni Frank Jame...


Mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo katikati akiwa na wakuu wapya wa wilaya za Arumeru Bwana Jerry Muro kushoto na kulia ni Frank James  Mwaisumbe wa wilaya ya longido mara baada ya kuapishwa leo katika ofisi ya mkuu wa mkoa Arusha tayari kwenda kuwatumikia wananchi katika maeneo waliyopangiwa 


Mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo wa tatu kutoka kulia akiwa na wakuu wa wilaya mbalimbali zilizopo mkoani Arusha mara baada ya kuwaapisha wakuu wapya wa wilaya za Arumeru na Longido
 
 
Mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo amewataka wakuu wapya wa wilaya za Arumeru na longido kuhakikisha wanatekeleza wajibu wao kwa kuzingatia ilani ya chama cha mapinduzi na ahadi za mheshimiwa Raisi Magufuli na kamwe wasitumie nafasi yao kumuonea mtu.

Akizungumza mara baada ya kuwaapisha wakuu hao wapya wa wilaya za Arumeru (Jerry Murro) na Longido ( Frank James  Mwaisumbe) amesema kuwa wakuu hao wa wilaya wamepewa jukumu kubwa na wanaheshima kubwa ambayo wanawajibika kuilinda kwa maslahi mapana ya nchi.

"Mmepewa majukumu makubwa kuna tabia ukipewa nafasi unaona kubwa ikizoea unaona ya kawaida mjuwe hii awamu ni tofauti lazima utendaji wenu uendane na katiba,sheria na miongozo ya serikali" alisema.

Alisema kuna  watu wakiteuliwa wanajiona  wana akili sana kuliko wanaowaongoza hivyo,katika ofisi kuna watu wa kuwasaidia hakuna ambaye hana kazi ofisini muwaheshimu ambao mtawakuta.
Mkuu mpya wa wilaya ya Arumeru, Jerry Muro,amewataka viongozi wilaya ya Arumeru ambao wanaona hawawezi kutekeleza Ilani ya uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) wapishane kabla ya hajaingia ofisini.

Akizungumza mara tu baada ya kuapishwa na Mkuu wa mko wa Arusha,Mrisho Gambo,Muro alisema ambao watakaoshindwa kutekeleza Ilani watapata taabu sana.

"Najua Rais John Pombe Magufuli anataka nini, nitashangaa kama watajitokeza watu wachache kutupinga" alisema

Muro alisema, miaka miwili iliyobaki anataka kuidhihirishia Arumeru ,Arusha na Tanzania inakwenda kubadilika.

"Nakuja Arumeru kuwatumikia na hii(Ilani ya uchaguzi) ndio nakuja kuitekeleza" alisema

Muro amemshukuru,Rais John Magufuli kwa kumuamini na  kumpa dhamana ya kwenda kuwatumikia wananchi wa Arumeru.

Alisema Rais John Magufuli ni zawadi na baraka kutoka kwa mungu kwani ndani ya muda mfupi amefanya mambo mengi makubwa .

Kwa upande wake,Mkuu mpya wa wilaya ya Longido,Frank James  Mwaisumbe  alimshukuru Rais Magufuli kwa kimteua na kuahidi kufanyakazi kwa nguvu zake zote,jasho lake na damu yake.

Mwaisumbe alisema amekuja kuweka chache ya maendeleo Longido pale ambapo wenzake wameishia ataendeleza.

"Nafahamu tayari mmefanya mengi mimi nimekuja kuendekeza na kuweka nguvu na kujifunza " alisema



About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top