PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: WADAU WA UTALII JIJINI ARUSHA WATOA MSAADA KUBORESHA HUDUMA YA AFYA
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
      WADAU wa utalii mkoani Arusha wamekabidhi msaada wa Vitanda 40 kumi  vikiwa ni vya kujifungulia wamama wajawazito na 30 ni ...
 
 
 
WADAU wa utalii mkoani Arusha wamekabidhi msaada wa Vitanda 40 kumi  vikiwa ni vya kujifungulia wamama wajawazito na 30 ni vya kulalia wagonjwa wa kawaida kwenye kituo cha afya cha Murieti jijini Arusha, ikiwa ni hatua ya kusaidia serikali kuboresha huduma za afya nchini .

Akikabidhi vifaa hivyo vyenye thamani ya shilingi milioni 29.8 kwa mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo,mkurugenzi wa kampuni mbili za utalii Kibo Guides na Tanganyika Wilderness Campus ,Willy Chambulo, amesema  kampuni zake zitaendelea kuchangia  sekta ya afya na elimu .

Kwa upande wake meneja mahusiano wa Hotel ya kitalii ya Mount Meru, Quen Mpeku,ambao wametoa msaada wa Taulo 250 zenye thamani ya shilingi milioni 8  
Amesema  wametoa msaada huo kusaidia wagonjwa watakaolazwa  kwenye kituo hicho cha afya ikiwa ni kusaidia kuboresha huduma ya afya kwenye Kituo hicho cha afya. 

Akipokea msaada huo mkuu wa mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo, amesema  serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Dakt John Magufuli, inaendelea na hatua ya kuboresha huduma ya afya nchini na Jijini Arusha.

Amesema kuwa hivi sasa jiji la Arusha linajenga hospital ya wilaya ambapo Raisi Magufuli amechangia shilingi bilioni 2,huku halmashauri ikiwa imetoa shilingi milioni 500.
 
Amesema kuwa pia serikali imetoa fedha za ujenzi wa hospital za wilaya za Longido na Ngorongoro  ambapo tayari zimeshatolewa shilingi bilioni 1 kwa ajili ya ujenzi huo.
 
Aidha amempongeza mkurugenzi wa kampuni hizo za Utalii kwa msaada wake  na kusema kuwa Chambulo,amekuwa mstari wa mbele katika kuchangia maendeleo ya mkoa wa Arusha.

Awali mganga mkuu wa mkoa wa Arusha Daktar Timoth Wanyonji, amesema  vifaa hivyo vimekabidhiwa kwa timu ya uendeshaji na  uboreshaji wa huduma ya afya ya mkoa na jiji la Arusha,ambapo mkakati uliopo ni kuendelea na kupunguza vifo vya wajawazito na watoto wakati wa kujifungua ikiwa ni hatua ya kuboresha huduma ya tiba na kinga.

Amesema vifo vya watoto na akina mama vinaendelea kupungua mwaka hadi mwaka kutokana na  kuboresha huduma za afya na kinga.
Kwa upande wake mkurugenzi wa jiji la Arusha,Athuman Kihamia,akipokea msaada huo amesema Kituo cha afya cha Mriet ni kipya hivyo kupatikana kwa vifaa hivyo kutaboresha huduma ya afya.

Ameongeza kuwa jengo la wagonjwa wa nje OPD   limekamilika kwa asilimia 90  na bado wanaendelea kukamilisha majengo mengine ikiwemo la chumba cha kuhifadhia maiti, wadi ya kujifungulia, maabara, ambapo yapo ujenzi wake umefikia 50 asilima.





 

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top