PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: MABANDA YA TAASISI ZA UHIFADHI TANAPA, FCF NA NCAA YAWAVUTIA WENGI MAONESHO YA NENANE SIMIYU
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
Wananchi mbalimbali wakipata maelezo na umuhimu wa utalii ndani ya mabanda ya utalii katika maonesho ya nanenane  Mkoa...








Wananchi mbalimbali wakipata maelezo na umuhimu wa utalii ndani ya mabanda ya utalii katika maonesho ya nanenane  Mkoani Simiyu yanakofanyika kitaifa mkoani hapa

Mabanda ya taasisi za uhifadhi za Shirika la hifadhi za Taifa(TANAPA),taasisi ya uhifadhi ya Friedkin Conservation Fund(FCF) na Ngorongoro yamekuwa vivutio vya wananchi wanaoshiriki Maonesho ya wakulima na wafugaji nane nane mwaka huu kitaifa mkoani Simiyu.

Taasisi za uhifadhi hizo ,Shirika la hifadhi za Taifa(TANAPA),Friedkin conservation Fund (FCF) na Mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro,wamekuwa wakitoa elimu ya uhifadhi ,vita dhidi ya ujangili na kuna ofa za kutembelea uhifadhi katika hifadhi za Taifa na mamlaka ya hifadhi Ngorongoro.

Meneja kitengo cha ujirani Mwema cha shirika la hifadhi za Taifa(TANAPA),Ahmed Mbugi alisema shirika hilo limejipanga kutumia maonesho haya kutangaza utalii.

Mbugi alisema katika maonesho hayo,TANAPA itatoa magari kuwapeleka watalii hifadhi za taifa za Serengeti kwa washiriki wa maonesho ya kitaifa mkoani Simiyu.

Alisema kwa wanaoshiriki maonesho mkoa wa Morogoro watapelekwa Hifadhi ya Taifa ya mikumi kwa kuchangia gharama.

Katika maonesho hayo,pia Taasisi binafsi za uhifadhi zitatoa huduma ikiwepo taasisi ya Friedkin conservation Fund(FCF) ambayo kwa mara ya kwanza itashiriki mwaka huu.

Meneja uhusiano wa Friedkin Conservation Clarence Msafiri alisema katika maonesho ya mwaka huu wanatoa elimu ya uhifadhi na vita dhidi ya ujangili.

"Pia tutahamasisha watanzania kwenda kutembelea vivutio vya utalii katika mapori ya akiba  ambayo tumewekeza ikiwepo eneo la makao kwa wakazi wa kanda ya ziwa" alisema

Mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro(NCAA) pia wanatumia maonesho hayo kupeleka watalii wa ndani ya mamlaka ya hifadhi kuona vivutio vilivyopo Ngorongoro.

Naibu Mhifadhi Mkuu wa Ngorongoro,Dk Maurus Msuha alisema magari maalum yameandaliwa kutoka Arusha hadi Ngorongoro kutembelea vivutio kwa malipo kidogo.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top