PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: ILO YAWAKENGEA UWEZO VIONGOZI WA VYAMA VYA WAFANYAKAZI,UHAMIAJI NA SERIKALI
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
Waziri wa Nchi,Ofisi ya Waziri Mkuu,Kazi,Vijana,Ajira na Wenye Ulemavu ,Profesa Joyce Ndalichako akifungua mkutano huo Washiriki wa mkutano...
Waziri wa Nchi,Ofisi ya Waziri Mkuu,Kazi,Vijana,Ajira na Wenye Ulemavu ,Profesa Joyce Ndalichako akifungua mkutano huo

Washiriki wa mkutano huo wakimsikiliza Waziri, Professa Joyce Ndalichako

Mshauri wa masula ya kiufudi wa shirika la Kazi la Umoja wa Mataifa(ILO) katika ukanda  wa Kusini mwa Afrika,Gloria Moreno Fontes akizungumza na waandishi katika mkutano wa uhamaji ajira.

Na: Andrea Ngobole, Arusha


Shirika la Kimataifa la Kazi Duniani(ILO)  limetaka watendaji katika utatu wa uhamaji nguvu Kazi na usimamizi uhamiaji kufanya Kazi  kwa ushirikiano ili kuwezesha wafanyakazi kufanya Kazi kutoka nchi moja hadi  nyingine.


Mshauri wa masula ya kiufudi wa shirika la Kazi la kimataifa(ILO) katika ukanda  wa Kusini mwa Afrika,Gloria Moreno Fontes akizungumza katika kikao Kazi cha wataalam vyama vya wafanyakazi, maafisa uhamiaji na idara za Kazi pamoja na waajiri alishauri uwepo ushirikiano baina yao.


Moreno amesema shirika hilo linawajengea uwezo vyama vya waajiri,Taasisi za serikali na vyama vya wafanyakazi ili kuondoa changamoto za uhamaji nguvu kazi kutoka nchi moja hadi nyingine.


"ILO  itaendelea kusaidia Tanzania ambayo ni miongoni mwa nchi zilizo katika mradi wa kuboresha Mazingira ya uhamaji nguvu kazi na masuala ya uhamiaji"amesema


Akifungua mkutano huo,Waziri wa Nchi,Ofisi ya Waziri Mkuu,Kazi,Vijana,Ajira na Wenye  Ulemavu ,Profess Joyce Ndalichako  amesema mkutano huo utawezesha usimamizi mzuri wa utatu wa uhamaji wa nguvu kazi  na usimamiaji uhamiaji kutoka nchi moja hadi nyingine.


Waziri Ndalichako alisema changamoto za wafanyakazi nje ya nchi zinaweza kupatiwa Suluhu Kama utatu huo ukifanyakazi vizuri.


" Tumekuwa tukiona wafanyakazi wanapopata shida ndipo wanakimbilia Ofisi za ubalozi lakini walipaswa kufuata sheria na taratibu wanapokwenda kufanyakazi"amesema


Profesa Ndalichako, amesema uhamaji nguvu kazi kutoka nchi moja hadi nyingine unapaswa kuzingatia Sheria na mikataba ya kimataifa.


Alisema mradi huo wa uhamaji nguvu pia unatekekezwa  na nchi  nyingine ambazo ni Kenya, Ethiopia,Uganda na Sudani Kusini .


Ofisa ofisi ya  Kamishna wa Kazi Zanzibar Amir Ally Amir alipongeza uwepo was mradi huo ambao utapunguza kero za wafanyakazi.



About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top