PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: WAZIRI WA KILIMO AZITAKA KAMPUNI ZA UWINDAJI WA KITALII KUONGEZA MICHANGO KWA JAMII
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
 Waziri wa kilimo Dr. Charles Tizeba akisaini kitabu alipotembelea Taasisi ya uhifadhi ya Friedkin conservation Fund,(FCF) inayomiliki ka...
 Waziri wa kilimo Dr. Charles Tizeba akisaini kitabu alipotembelea Taasisi ya uhifadhi ya Friedkin conservation Fund,(FCF) inayomiliki kampuni za uwindaji wa kitalii,katika maonesho ya Nanenane kitaifa mkoa Simiyu mapema jana

 Waziri wa kilimo Dr. Charles Tizeba akizungumza na watendaji wa Taasisi ya uhifadhi ya Friedkin conservation Fund,(FCF) inayomiliki kampuni za uwindaji wa kitalii,katika maonesho ya Nanenane kitaifa mkoa Simiyu mapema jana


 Waziri wa kilimo Dr. Charles Tizeba akizungumza na watendaji wa Taasisi ya uhifadhi ya Friedkin conservation Fund,(FCF) inayomiliki kampuni za uwindaji wa kitalii,katika maonesho ya Nanenane kitaifa mkoa Simiyu mapema jana
 Waziri wa kilimo Dr. Charles Tizeba akizungumza na watendaji wa Taasisi ya uhifadhi ya Friedkin conservation Fund,(FCF) inayomiliki kampuni za uwindaji wa kitalii,katika maonesho ya Nanenane kitaifa mkoa Simiyu mapema jana

Mwandishi wetu.
Waziri wa Kilimo,Dk Charles Tzeba amezita kampuni za uwindaji wa kitalii nchini,kuongeza michango ya fedha wanazotoa kwa jamii ambayo inazunguka mapori ya akiba nchini.

Akizungumza na watendaji wa Taasisi ya uhifadhi ya Friedkin conservation Fund,(FCF) inayomiliki kampuni za uwindaji wa kitalii,katika maonesho ya Nanenane kitaifa mkoa Simiyu,Dk Tzeba alisema kuna kampuni zinapata fedha nyingi lakini uchangiaji jamii ni ndogo.

"Nyie najua mnafanya vizuri lakini wenzenu katika maeneo mengine hadi wamefikia hatua ya kuwachagulia miradi wananchi" alisema.

Hata hivyo,Afisa uhusiano wa FCF,Clarence Msafiri alisema kampuni zilizo chini ya Taasisi hiyo,zimekuwa zikitoa kwa jamii asilimia 20 ya mapato yao kila mwaka.

Alisema kampuni zao ikiwepo Mwiba Holding na TGTS na walizowekeza wilayani Meatu pori la Akiba la Maswa na Makao licha ya kutoa michango ya kijamii pia kwa mwaka wanatoa kwa vjiji zaidi ya sh 610 million kama kodi ya pango.

Naye Meneja ujirani Mwema wa kampuni ya Mwiba Holdings Alfred Mwakivike alisema kampuni hiyo kabla ya kusaidia miradi imekuwa ikipata maelekezo ya halmashauri.

"Miradi ambayo tunaitekeleza ambayo ina thamani zaidi ya sh 2. bilioni yote imeidhinishwa na halmashauri ya Meatu" alisema.

Taasisi ya Friedkin inashiriki maonesho ya nanenane kwa mara ya kwanza ili kuhamasisha uhifadhi,kupiga vita ujangili lakini kuonesha umuhimu wa mahusiano ya uhifadhi na kilimo.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top