PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: MTOTO ANDREW ALIYEANGUKIWA NA UKUTA NA KUPATA MATATIZO KATIKA MFUMO WA NJIA YA MKOJO ANAHITAJI MSAADA WAKO WA HARAKA!!
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
Mama mzazi wa Andrew ,Janeth Chacha akimfanyia usafi wa mfuko ambao hutumika kutolea na kuhifadhi haja  ndogo  kwa mtoto wake Andre...

Mama mzazi wa Andrew ,Janeth Chacha akimfanyia usafi wa mfuko ambao hutumika kutolea na kuhifadhi haja  ndogo  kwa mtoto wake
Andrew Jacob akiwa na wazazi wake  Jacob Rohole na mama yake  Janeth Chacha  nyumbani kwao mtaa wa Nyamatare,Musoma mjini

Mtoto AndrewJacob akiwa na mfuko maalumu kwaajili ya kutolea haja  ndogo

'HERI KUFA KULIKO KUISHI'
*Ni kauli ya mtoto Andrew Jacob
*Anaiyeishi na mpira  wa kutolea haja  ndogo
*Ni baada ya kuangukiwa na ukuta
*Njia ya mkojo  yapishana,aomba  msaada wa matibabu

"HERI kufa  kuliko kuishi,napata maumivu makali sana,muwasho usiokoma sehemu za siri jambo ambalo linanifanya nikose raha"

" Maisha yangu yamekuwa  tia  maji tia  maji leo  mzima kesho mgonjwa...hospitali  imekuwa  nyumbani kwangu hali hii siipendi  basi tu sina namna ninaomba wasamaria wema wanisaidie kuokoa maisha yangu bado safari ni ndefu ya kuweza kutimiza ndoto zangu kimaisha"

Haya ni  maneno yaliyojaa kigugumizi na maumivu makali kutoka kwenye kinywa  cha mtoto Andrew Jacob(7) mwanafunzi wa darasa la  kwanza katika shule ya Msingi Nyamatare iliyopo Musoma Mjini mkoani Mara wakati wa mahojiano na mwandishi wa Makala haya.

Akielezea masahibu yaliyompata hadi kufikia hatua ya kuomba msaada kwa wasamaria wema,Mtoto Andrew anasema Ana kumbuka ilikuwa jioni ya Desemba 13,2016 ambapo alikuwa akicheza mchezo maarufu kwa jina la  kombolela na wenzake aliangukiwa na ukuta wa nyumbani kwao ulimsababishia kuvunjika kiuno,mguu wa kushoto na njia ya mkojo  kupishana.

Mtoto Andrew anasema kuwa wakati ajali hiyo ya kuangukiwa na ukuta ikitokea wazazi wake ambao ni wajasiriamali wa kuuza matunda  hawa kuwepo nyumbani hivyo msaada wa kwanza aliupata kutoka kwa majirani ambao walimtoa kwenye ukuta uliomwangukia na kisha kuwapigia simu wazazi ambao ni Jacob Rohole na Janeth Chacha.

Andrew anasema wakati huo wote alikuwa hajitambui kutokana na kupoteza fahamu na wazazi wake walipofika nyumbani walimchukua na kumkimbiza katika hospitali  ya mkoa ambako alipatiwa matibabu ya awali na siku iliyofuatia alihamishiwa Hospitali  ya Bugando iliyopo mkoa Mwanza.

Baada ya kuwasili Bugando alipolewa vizuri na kuanza matibabu ambapo  siku chache baadaye alifanyiwa upasuaji wa njia ya mkojo...hapa Andrew anashindwa kuendelea kuzungumza kutokana na kigugumizi na maumivu makali hivyo kunikazimu kuendelea na mazungumzo na baba mzazi Rohole.

Baba huyo wa mtoto Andrew anaeleza kuwa baada ya upasuaji wa njia ya mkojo bado hali haikuwa ya kuridhisha sana  kwani mtoto wake hakuweza kujisaidia  kama  awali badala yake alilazimika kutumia mpira  maalumu  ambao ulikuwa ukimsababishia maumivu makali.

Anasema hali hiyo ilidumu kwa miezi mitatu waliyolazwa hoapitalini  hapo  na ndipo Daktari aliyekuwa akimuhudumia ( jina linahifadhiwa) alipowapa rufaa ya kwenda hospitali  ya KCMC iliyopo Moshi mkoani Kilimanjaro kwa  matibabu zaidi Machi 2017.

Hata hivyo baba huyo wa  mtoto anaeleza kuwa kutokana na ukata uliokuwa  ukimkabili ilimlazimu kurejea nyumbani Musoma kwaajili ya kujipanga kutafuta fedha kwaajili ya safari ya matibabu ya kuelekea KCMC Moshi.
Baada ya miezi kadhaa ndipo alipo kwenda KCMC na kuandikiwa kipimo cha X- ray ambacho kwa wakati huo kilikuwa na hitilafu hivyo kulazimika kwenda Arusha ambako nako alikutana na tatizo hilo hilo katika hospitali alizokwenda ikiwemo Mount Meru ambayo ni ya mkoa.

Rohole anabainisha kuwa alizunguka sana  na mtoto Andrew hadi walipofanikiwa kufanyiwa kipimo  hicho katika kituo cha X- ray Center jijini Arusha na kurudi KCMC huku wakiwa hoi kwa uchovu.

Wangali wakiwa katika hali hiyo ya uchovu na maumivu makali kwa mtoto Andrew walifanikiwa kuonana na daktari  ambaye baada ya kusoma picha za vipimo vya X- ray aliweka bayana kwamba tatizo la  mtoto huyo ni vigumu  kutibika kwani hakukuwa na wataalamu hivyo warudi Musoma hadi Agosti 2017  ambako KCMC ingekuwa  na wataalamu kutoka nje ya nchi ambao wangeweza  kumtibu kijana wake.

" Sikuamini nilichokisikia,nilinyong'ea lakini sikuwa na namna nyingine zaidi ya kurudi nyumbani  na hilo ndilo linalonisukuma kuomba msaada kwaajili ya mtoto wangu aweze kwenda kutibiwa nje ya nchi "anasisitiza Rohole
Hata hivyo Rohole anaeleza kuwa mara baada ya kurudi Musoma bado hali ya Andrew haikuwa ya kuridhisha na hata mahudhurio ya shule hayakuwa mazuri kwani siku zingine huamka akiwa mgonjwa sana na kulazimika kumkimbiza hospitali.

Ndipo kama  familia wakafikia maamuzi ya kwenda kwa Mkuu wa Wilaya ya Musoma mjini Dk Vincent Anney kumweleza juu ya tatizo  la  mtoto wao na hali duni ya kimaisha waliyo nayo  hivyo kupatiwa kibali cha kuchangiasha fedha kwaajili ya matibabu ya mtoto Andrew.

" Pamoja na kwamba tuna kibali cha kuchangisha fedha kwaajili ya mtoto Andrew lakini mwitikio ni mdogo sana na hali  yake kiafya nazidi kuzorota siku hadi siku " anaeleza Rohole kwa masikitiko makubwa
Pamoja na mambo mengine Rohole anasisitiza kuwa kipato chake ni duni kwani hukosa hata sh 50,000 kwa mwezi  kwaajili ya kununua vifaa vya kumsaidia Andrew kupata haja  mdogo  hivyo kumlazimu mama wa mtoto huyo kufua  vya zamani jambo ambalo si salama na ni hatari kiafya.

"Itoshe kusema Andrew anateseka sana hivyo Kama mzazi ambaye ninaishi maisha duni ninaomba  msaada kwa wasamaria wema  ili akatibiwe nchini India ambako kwa makadirio ya chini kiasi cha fedha kinachohitajika sio chini ya shilingi.milioni 50" anahitimisha baba wa mtoto Andrew

Naye mama mzazi  wa mtoto Andrew, Janeth anasema tangu mtoto wake apate ajali hiyo ya kuangukiwa na ukuta  familia imeyumba sana kimapato hivyo anaomba msaada kwa wasamaria wema  wa kupatiwa fedha na hospitali nchini  India kwaajili ya matibabu ya haraka ya kijana wake huku akimtaja rais  John Magufuli na kumwomba aitazame familia hiyo kwa jicho la  tatu kwani siku za hivi karibuni amejitoa sana  katika kusaidia  wagonjwa.
Kauli ya anyosoma Andrew

Kwa upande wake Mwalimu wa darasa wa mtoto Andrew,Dainess Mwingi anakiri kwamba licha  ya tatizo alilo nalo mtoto huyo lakini Ana uwezo mkubwa sana  kiakili ikilinganishwa na watoto wengine darasani.
Anasema wakati mwingine hata kama  anaumwa hutoroka nyumbani na kwenda shule hivyo hulazimika kumrudisha nyumbani ili apate muda wa kupumzika  na kutazama afya yake kwanza.

" Mtoto Andrew anahitaji msaada wa haraka kwaajili ya matibabu ili aweze kurejea katika hali yake si jambo jema tena mwakani akirudia darasa  kama  ilivyotokea mwaka jana ambapo alishindwa kuhudhuria masomo mwaka mzima " anasisitiza Mwl wa mtoto Andrew

Andrew amezaliwa kwenye familia ya kawaida yenye  watoto watano huku yeye akiwa ni mtoto wa nne  kuzaliwa.
Ni familia inayoishi kwenye nyumba ambayo hata ujenzi wake haujakamilika  kutokana na hali ngumu ya ukata .

Wazazi wa mtoto huyo ni wajasiriamali wadogo wa kuuza matunda ambao hivi sasa  ukata umeigubika familia hiyo kiasi cha kushindwa kujikimu kimaisha tangu Andrew alipopata ajali iliyomsababishia hali aliyo nayo  hivi sasa.
Hivi sasa  ni familia inayojiendesha kwa biashara ya mali  kauli katika matunda ambayo Wazazi hao wamejikita na hivi karibuni walijikuta wakiingia katika madeni ya zaidi ya mil 2 baada ya kutapeliwa na watu waliodai kutaka kuwasaidia  ili waweke pesa kwenye akaunti ya mtoto Andrew aweze kupata matibabu haraka.

Kifupi ni familia inayohitaji msaada wa haraka ili mtoto Andrew aweze kutibiwa nchini India na kupona ili wazazi wake warejee katika shughuli za uwajibikaji na kutunza familia ipasavyo.


About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top