PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: Kauli ya Profesa Jay Kuhusu Wasanii Walioenda Jimboni Kupinga Ubunge Wake
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
  Mbunge wa Jimbo la Mikumi kupitia CHADEMA ambaye pia ni msanii wa 'hip hop', Joseph Haule (Profesa Jay) amese...



Mbunge wa Jimbo la Mikumi kupitia CHADEMA ambaye pia ni msanii wa 'hip hop', Joseph Haule (Profesa Jay) amesema hana kinyongo na wasanii  wote waliokwenda jimboni kwake kipindi cha uchaguzi oktoba 25, 2015 kwa ajili ya kumpinga.


Msanii huyo kupitia ukurasa wake wa kijamii instagram ameandika maneno machache yanawagusa moja kwa moja wasanii wenzake waliokuwa nje ya chama hicho kuwa amewasamehe ila amewataka wajiongeze kwa maana sanaa inahitaji umoja.


"Nilishawasemehe wasanii wenzangu waliokuja jimboni kupinga Ubunge wangu mabasi kwa mabasi,  jiongezeni wanangu. Asante wana Mikumi kwa kuwa na imani kwangu, sanaa yataka umoja nitakubeba ukianguka". Ameandika Profesa Jay


Kwa upande mwingine msanii huyo amewataka mashabiki na wapenzi wa muziki wake wakae tayari kupokea mzigo mpya siku ya kesho Jumatano unaotarajiwa kupewa jina la 'kibabe'.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top