PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: SHIMMUTA YAPATA MABINGWA VISHALE, POOL TABLE JIJINI ARUSHA.
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
Mchezaji wa Vishale wa timu ya Bodi ya Mikopo ya Elimu ya juu Zahra Kitala akiwa kwenye moja ya mchezo huo katika mashindano ya SHIM...

Mchezaji wa Vishale wa timu ya Bodi ya Mikopo ya Elimu ya juu Zahra Kitala akiwa kwenye moja ya mchezo huo katika mashindano ya SHIMMUTA yanayoendelea jijini Arusha. Picha na Yohana Challe

NA; YOHANA CHALLE.
ARUSHA.

Mashindano ya Mashirika ya Umma, Taasisi na Makampuni Binafsi (SHIMMUTA) yanayojumuisha jumla ya michezo 12 yanayoendelea jijini hapa yameanza kutoa mabingwa kwa baadhi ya michezo ambapo imeshuhudiwa timu Ya NEMC ikifanikiwa kuibuka mabingwa katika mchezo wa Vishale (Darts) kwa upande wa wanawake.

NEMC walifanikiwa kutangazwa washindi baada ya kuwatoa  wapinzani wao katika mchezo wa fainali , timu ya chuo kikuu Ardhi ambao waliambulia nafasi ya pili huku nafasi ya tatu ikiwaendea timu ya Bodi ya mikopo ya Elimu ya juu.

Kwa upande wa  mchezo wa Pool Table  kwa wanaume  Mshindi wa kwanza iliwaendea  shirika la viwango nchini TBS, nafasi ya pili kushikiliwa na  chuo cha ufundi Arusha (ATC) Huku Nafasi ya tatu ikiwaendea Shirika la hifadhi la mazingira Taifa (NEMC).

Katika michezo mingine ikiwemo riadha inatarajiwa kufanyika siku ya ijumaa ambapo washiriki wataweza kukimbia mita 100,200 na 400,na Michuano hiyo inatarajia kufika tamati Novemba 30 .

Aidha mbali na  michezo hiyo ,pia kumekuwa na taarifa ya baadhi ya timu shiriki kukata rufaa kwa kamati tendaji ya SHIMMUTA zikipinga baadhi ya timu kuhusisha wachezaji ambao ni mammluki.

“Kweli sisi kama kamati ya SHIMUTA tumepokea malalamiko kutoka timu ya shirika la maendeleao ya Petroli nchini (TPDC ) Katika mchezo wa mpira wa miguu, ambayo imekata rufaa  dhidi ya timu ya bodi ya mikopo ya Elimu ya juu  wakilalamikia  kuchezesha wachezaji 6 ambao sio wahusika yaani Mamluki” alisema katibu wa SHIMMUTA Award Safari.

Alieleza kuwa  mara baada ya Uchunguzi kukamilika dhidi ya malalamiko hayo yaliyotolewa na timu ya TPDFC kamati ya Nidhamu itatoa majibu juu ya tuhuma zilizotolewa ambapo sheria za mashindano zitachukua nafasi yake.

Michezo mingine ikiwemo Mpira wa Miguu,Mpira wa pete,Mpira wa kikapu  itaendelea leo Ijumaa katika viwanja vya General Tyre katika hatua za robo fainali.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top