PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: PAMOJA NA MAMBO YA ESCROW ACCOUNT KUTAWALA NCHINI> TANZANIA YAPATA ALAMA YA POINT TANO KATIKA MASUALA YA UONGOZI NA UTAWALA BORA.
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
   Naibu Waziri wa Fedha, Adam Malima, akizungumza wa...


 Naibu Waziri wa Fedha, Adam Malima, akizungumza wakati akiifungua semina ya Kujadili masuala ya Uwajibikaji katika kuleta maendeleo kwa jamii nchini, Dar es Salaam jana. Semina hiyo iliyoandaliwa na wizara hiyo, imefadhiliwa na Benki ya Maendeleo Afrika (ADB)
  Mwakilishi Mkazi wa ADB, Tonia   Kandiero  wakati  semina  ya Kujadili masuala ya Uwajibikaji katika kuleta maendeleo kwa jamii nchini, Dar es Salaam jana. Semina hiyo iliyoandaliwa na wizara hiyo, imefadhiliwa na Benki ya Maendeleo Afrika (ADB).
 Baadhi ya wadau wa semina hiyo .
 Naibu Waziri wa Fedha, Adam Malima, akizungumza wakati akiifungua semina ya Kujadili masuala ya Uwajibikaji katika kuleta maendeleo kwa jamii nchini, Dar es Salaam jana. Semina hiyo iliyoandaliwa na wizara hiyo, imefadhiliwa na Benki ya Maendeleo Afrika (ADB).
Na Magreth Kinabo, MAELEZO
TANZANIA imepata alama ya pointi tano katika  masuala ya uongozi bora  kwenye ripoti ya  maendeleo ya ukuaji wa uchumi wa nchi za Afrika(Afrika For Results) ya mwaka huu.
Hayo yalisemwa  leo na Waziri wa fedha,Adam Malima  wakati  akizungumza katika ufunguzi wa semina ya siku nne wa  kutathimini  ripoti  hiyo kwa  nchi ya Tanzania ukilinganisha na tafiti za nchi zingine za Afrika unaoendelea kwenye hoteli ya Kunduchi Beach  jijini Dares Salaam.
“ Katika ripoti hii  kipimo cha alama  zilizotumika ni 0-5 , hivyo Tanzania imefanya vizuri katika masuala ya uongozi bora kwa kupata alama hiyo,” alisema Malima .
 Katika ripoti iliyoandaliwa na Benki ya Maendeleo ya Afrika(ABD) ikishirikiana na Serikali ya Tanzania ambayo imetaja maeneo sita ya kuzingatia katika kuhakikisha ukuaji wa uchumi unafika kwa wananchi wote wakiwemo wa  kawaida kwa kuzingatia hilo na mengineo.
Aliyataja maeneo hayo   ambayo ni  uwajibikaji  kwa alama 4.1.  uwezo wa kitaasisi  alama 4, mikakati ya kibajeti  alama  2.9,  mipango yenye kuleta matokeo alama  4.5 na matumizi ya Tehama  alama 2.3.
Naibu Waziri huyo  alisema ili  kutengeneza fursa sawa katika ukuaji wa uchumi  ni muhimu kuboresha viashiria vya kukua kwa uchumi na kupunguza umaskini.
 “Wananchi wa kawaida  wanaambiwa kuwa uchumi umepanda kwa asilimia saba lakini, baadhi yao  hali yao kimaisha  bado ni duni na wanashindwa kuamini ukuaji huo hivyo  kwa kutumia viashilia hivyo tunaweza kugundua na kuboresha baadhi ya maeneo ambayo yameonekana kuwa chanzo cha kutowafikia wananchi wa kawaida,”alisema Malima.
Wadau hao  katika mkutano huo watajadili   njia ambazo zitakazo saidia kuwafikia wananchi wa kawaida kukua kiuchumi ili kufikia Dira ya Taifa ya Maendeleo ya mwaka 2025 ya kuwa nchi yenye uchumi wa kati.
Kwa  upande wake Mwakilishi Mkazi wa ADB, Tonia   Kandiero  alisema  wadau  hao  watajadili  ripoti  hiyo katika  mkutano  huo  wa  kutathimini  ripoti  hiyo kwa  nchi ya Tanzania  kwa siku nne ,  na kulinganisha na nchi zingine za Afrika unaoendelea kwenye hoteli ya Kunduchi Beach  jijini Dares Salaam.
 Akitoa uzoefu wake katika nchi ya Zimbabwe, Erick  Zinyengere, ambaye ni Meneja wa Ushauri alisema ili kuweza kuleta mafanikio ya kimaendeleo katika miradi mbalimbali ni vema kushirikisha wananchi  katika hatua ya kwanza hadi ya mwisho.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top