Home
»
»Unlabelled
» POLISI ARUSHA WAWAAANGUKIA SSRA
ASKARI Polisi mkoani Arusha, wameiomba Mamlaka ya Udhibiti wa
Mifuko ya Hifadhi ya Jamii (SSRA) kuweka mazingira yatakayowawezesha
kuhamisha mafao yao kutoka mfuko mmoja kwenda mwingine.
Akizungumza katika warsha iliyoandaliwa na SSRA, Inspekta Joseph
Labia, alisema uzoefu unaonyesha kuna ugumu wa kuhamisha mafao kutoka
mfuko mmoja kwenda mwingine.
“Kuna mifuko ina mafao mazuri kuliko mwingine na wengi tungependa
kuwa na hiyari ya kuhamisha mafao yetu, lakini kuna ugumu wa kuruhusiwa
kuhamisha. Tunaomba SSRA muweke mazingira mazuri kwa hili kuwezekana,”
alisema Inspekta Labia.
Awali Mkurugenzi SSRA, Ansgnar Mushi, alisema hivi sasa wanafanya
utaratibu wa kuoanisha kanuni ya ukokotoaji wa mafao ya wastaafu iwe
moja kwa mifuko yote, ili kuwezesha watu kuwa huru kuhamisha mafao yao.
Semina hiyo ilikuwa na lengo la kutoa uelewa wa kutosha kuhusu
shughuli za mamlaka hiyo pamoja na uendeshwaji wa sekta ya hifadhi
jamii nchini.
About Author

Advertisement

Recent Posts
- The Maasai Families in Longido District allegedly use baptism ceremonies to conceal FGM practices17 Sep 20240
By our Reporter in Longido Some Maasai families in Longido District, Arusha Region ar...Read more »
- Tanzanian Shillings 6.56 Trillion Investment in the JNHPP Project Bears Fruits for the Nation14 Sep 20240
By Our ReporterThe Public Investments Committee (PIC) of Parliament visited the construction site of...Read more »
- 35 teams set to battle in Chem Chem Cup 2024: Sh78 million up for grabs10 Sep 20240
By Mussa Juma, MaipacBabati. A total of 35 teams will participate in the 2024 Chem Chem Cup, costin...Read more »
- Mwiba holdings Donates house for Health Workers and 194 bicycles to Meatu students.29 Aug 20240
By Our Staff Writer in MeatuMwiba Holdings Ltd, a tourism and conservation investment company ...Read more »
- Mount Kilimanjaro porters' jobs in jeopardy due to foreign influence and controversial practices29 Aug 20240
KPAP's influence has shifted the tourism market, with foreign agents favoring their affiliates over ...Read more »
- Tanzania ramps up health education amid Mpox threat25 Aug 20240
By Staff WriterIn a bold move to safeguard Tanzania from the looming threat of Mpox, the Ministry o...Read more »
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.