PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: FARU WA HIFADHI YA SERENGETI KULINDWA KWA GHARAMA YA SHILINGI BILIONI 2.5
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
    Mwandishi wetu,Arusha.   Vita dhidi ya ujangili wa Faru, imeendelea kushika kasi na sasa Faru wa sereng...







 
 
Mwandishi wetu,Arusha.
 
Vita dhidi ya ujangili wa Faru, imeendelea kushika kasi na sasa Faru wa serengeti,wataanza kulindwa  na vifaa maalum vya kielekroniki katika mradi ambao utagharimu zaidi ya shilingi 2.5 bilioni.


Mradi huo,unafadhiliwa na shirika la uhifadhi za Friedkin conservation Fund(FCF) kwa kushirikiana na  shirika la  Frunkfurt zoological society na kusimamiwa na shirika la hifadhi za taifa nchini(TANAPA) na taasisi ya utafiti wa wanyamapori(TAWIRI).

Mratibu wa Mradi wa uhifadhi wa Faru katika hifadhi ya Taifa ya Serengeti, Philbert Ngoti alisema, vifaa hivyo  ambavyo vitawezesha Faru wa Serengeti kuwa salama zaidi.

Alisema Faru wa Serengeti wanafungwa vifaa vya aina mbili,vya kielekroniki VHF transmitter  ambacho kinawezesha kuwafatilia walipo kila siku na pia wanafungwa katika mguu wa kulia kifaa cha kisasa cha LoRa collar ambacho pia kinafatilia na kuonesha mienendo yao kila siku.
 
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Japhet  Hasunga, alisema zoezi la ufungwaji wa vifaa ya utambuzi na usalama kwa Faru ni muhimu sana katika kuimarisha vita dhidi ya ujangili.
 
Alisema zoezi hilo pia litasaidia kuongeza ufatiliaji wa faru,wanyama ambao wapo hatarini kutoweka duniani na sasa  kila siku watajulikana wapo wapi, wanakula nini, wanaumwa ama wanamatatizo na hivyo kuchukuliwa hatua.
 
Meneja miradi wa shirika la Frunkfurt Tanzania, Rian Habuschagne, alisema katika mradi huo ambao ni mara ya kwanza kufanyika nchini, pia kumejengwa minara ya mawasiliano katika maeneo yote ya mapito ya Faru.

Alisema zoezi la kufungwa vifaa hivyo linasimamiwa na watafiti na wahifadhi maarufu wa Faru barani Afrika, wakiongozwa na Pete Morkel na wanatarajia Faru wote wa serengeti kufungwa vifaa hivyo.

"hili zoezi linagharama kubwa tunawashukuru Friedkin Conservation Fund kwa msaada mkubwa wa fedha na helkopta, pia Frunkfurt ,TANAPA na taasisi ya utafiti wa wanyamapori(TAWIRI)"alisema.
 
HIfadhi ya Taifa ya Serengeti ni moja ya maeneo yenye Faru wengi kwa sasa hapa nchini kutokana na kuimarishwa ulinzi.


About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top