PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: WATUHUMIWA WANNE WA UJANGILI WAKAMATWA NA MTAMBO WA KUTENGENEZA MAGOBOLE
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
  Watuhumiwa manne wa ujangili wamekamatwa na bunduki aina ya gobole na mtambo wa kutengeneza silaha hizowilayani uvinza mkoani Ki...
 

Watuhumiwa manne wa ujangili wamekamatwa na bunduki aina ya gobole na mtambo wa kutengeneza silaha hizowilayani uvinza mkoani Kigoma.

Akizungumza na waandishi wa habari meneja wa taasisi ya uhifadhi ya Friedkin Conservation Fundi (FCF) Uvinza,mkoani Kigoma Audax Karurama alisema kukamatwa watuhumiwa hao wa ujangili ni matokeo ya kazi ya intelijensia baina ya askari Friedkin Conservation Fund ambao wanamiliki kitalu katika eneo hilo na askari ya wanyamapori.

Karurama alisema, katika maeneo ya  Uvinza Msebehi  kwa ushirikiano na askari wa Wanyamapori eneo la kifura walifanikiwa kukamata mtuhumiwa wa ujangili j akiwa na silaha aina ya  gobore na  Fundi wa kutengeneza magobore. .

Alimtaja mtuhumiwa Huyo ambaye tayari anashikiliwa na jeshi la polisi kuwa ni Majaliwa Ramadhan(59) Mkazi wa kibaoni uvinza. 

"Huyu mtuhumiwa tumemkuta pia na Goroli 20 Baruti  1/4 kilo, Mitego miwili ya waya na nyuzi za katani" alisema

 Alisema katika  msako huo wamefanikiwa kumkamata fundi wa magobole  ,Laurent Sungura(55) akiwa na mtambo wake maeneo  mlubanga -basanza .

Katika msako huo eneo la Uvinza walikamata watuhumiwa wawili Wino Emily na Zakia sinzi  wote wa kijiji cha mvinza  wakiwa na gobole.

"Tumewafuatilia sana kwa ujanja wao wakaenda kusalimisha gobore kwa mwenyekiti wa kijiji chao wakabaki na Smg Kwa hiyo bado Tunawafuatilia kwa karibu ili kukamata hiyo silaha yao" alisema.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top