PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: WILAYA YA MONDULI YAZINDUA JUKWAA LA UWEZESHAJI WANAWAKE
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
Afisa Ustawi wa Jamii Wilaya ya Monduli Rose Mhina  akifafanua jambo katika uzinduzi wa jukwaa la Uweshaji wa Wanawake kiuchumi.Picha na ...
Afisa Ustawi wa Jamii Wilaya ya Monduli Rose Mhina  akifafanua jambo katika uzinduzi wa jukwaa la Uweshaji wa Wanawake kiuchumi.Picha na Ferdinand Shayo

Mkuu wa Wilaya ya Monduli Iddi Hassan akizungumza katika uzinduzi wa Jukwaa la Uwezeshaji wanawake Kiuchumi Ambalo lilihudhuriwa na wanawake kutoka kila kata ya Wilaya hiyo.Picha na Ferdinand Shayo


Viongozi wa Wilaya wa Jukwaa la Uwezeshaji Wanawake Kiuchumi wakiwa kwenye mkutano.Picha na Ferdinand Shayo

Baadhi ya Wanawake kutoka wilaya ya Monduli wakifuatilia kwa makini mkutano.Picha na Ferdinand Shayo


Na Ferdinand Shayo,Arusha.

Wilaya ya Monduli imezindua rasmi jukwaa la Uwezeshaji wanawake kiuchumi ambapo jukwaa hilo linatarajia kusaidia vikundi vya kinamama vyenye uelekeo wa Ushirika ikiwemo Vikundi vya uzalishaji mali,ujasiriamali pamoja na Vikoba.

Akizungumza katika uzinduzi wa Jukwaa hilo Mkuu wa Wilaya ya Monduli Iddi Hassan alisema kuwa serikali ina jukumu la kuwawezesha wanawake kwa kupitia fedha zinazotengwa na halmashauri kwa ajili ya mikopo ya vikundi vya kinamama ili waweze kuinuka kiuchumi.

Iddi amewataka Wanawake hao kuzalisha bidhaa bora pamoja na kuzifungasha vyema ili waweze kupata masoko ya uhakika ndani na nje ya nchi.

Afisa ustawi wa Jamii Wilaya ya Monduli Rose Mhina  amesema kuwa jukwaa la Uwezeshaji wa Wanawake litawasaidia wajasiriamali na vikundi vidogo vidogo ikiwemo VIKOBA katika kuunganisha nguvu kwa pamoja na kutumia fursa ya kukopa fedha ili kujiendeleza kiuchumi.

“Tumefanya uchaguzi na kupata wawakilishi kila kata itatusaidia kufuatilia kwa karibu na kuhamasisha masuala ya uwezeshaji wa wanawake kwa urahisi ili kuwafikia wanawake wote katika wilaya ya Monduli” Alisema Rose

Mwenyekiti wa Baraza la Uwezeshaji wa Wanawake mkoa wa Arusha  Roda Msemwa alisema kuwa Jukwaa hilo lina jukumu ya kuhamasisha shughuli za uzalishaji pamoja namna ya kuwawezesha kiuchumi ili waweze kuondokana na umasikini katika kaya zao.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top