Home
»
yanayojiri ARUSHA
» USAJILI VITAMBULISHO VYA TAIFA WASHIKA KASI MKOA WA ARUSHA, WAANDISHI KUTOKA VYOMBO VYA HABARI WATEMBELEA VITUO VYA USAJILI
Kaimu Mkuu wa Kitengo cha
Mawasiliano (NIDA) Bi. Rose Joseph (mwenye miwani) akizungumza na baadhi
ya waandishi wa Vyombo vya Habari vya Televisheni na Magazeti
walipotembelea kituo cha usajili cha Sombetini, Arusha mjini kuangalia
shughuli za kuwasajili wananchi zinazoendelea kituoni hapo.
Wananchi wakiendelea kupata huduma
za usajili kabla ya kupigwa picha kama wanavyoonekana pichani. Wananchi
hao ambao ni kutoka Kata ya Sombetini wamekuwa wakijaziwa fomu na
kugongewa mihuri na wenyeviti kwenye mitaa wanayoishi kabla ya
kusajiliwa kwenye mfumo wa NIDA.
Hapa ni Mwenyekiti wa mojawapo ya
mitaa ya Kata ya Sombetini (mwenye kofia) akigonga mhuri kwenye fomu ya
mwananchi kuthibitisha kumtabua, na mkazi wa eneo lake.
Moja ya mashine aina ya BVR ikiendelea kuwasajiliwa wananchi wa Kata ya Sinoni waliopanga foleni kupata huduma ya Usajili.
Baadhi ya wakazi wa Kata ya Sinoni
Arusha wakiwa kwenye foleni ya kupigwa picha baada ya kukamilisha hatua
za awali za Usajili ambazo ni kujaza fomu za maombi na kuthibitishwa na
Idara ya Uhamiaji.
Akina mama pamoja na jukumu la
malezi wamejitokeza kusajiliwa kama anavyoonekana pichani mmoja wa
akinamama wa Kata ya Sinoni akiwa amembeba mtoto wake mkono mmoja na
mkono mwingine akiwa anaendelea na hatua za usajiliwa.
…………….
Baadhi ya waandishi wa Habari
kutoka vyombo mbalimbali vya Habari zikiwemo Televisheni na Magazeti
Jana walitembelea vituo vya Usajili mkoa wa Arusha kuona hatua za
usajili na mwitikio wa wananchi katika kupata haki yao msingi ya
kikatiba ya kusajiliwa.
Wananchi wa Mkoa wa Arusha
wameendelea kujitokeza kwa wingi kujisajili Vitambulisho vya Taifa; huku
idadi ya Kata za Usajili zikiongezeka. Moja ya Kata iliyoanza Usajili
jana kwa upande wa Wilaya ya Arusha mjini inaendelea kuwasajili wananchi
katika Kata ya Themi, Sekei, Sombetini na wameongeza Kata nyingine ya
Sinoni.
Wilaya ya Monduli inakamilisha
usajili kwenye Kata za Monduli Mjini, Monduli Juu na Engutoto;
ikijipanga kuendelea na Kata za Lashaine, Sepeko, Meserani na Mfereji.
Kwa Upande wa Arumeru Kata zinazofanya Usajili ni Musa, Ambureni,
Leburuki, Imbasenyi na Ngabobo, Longido ni Kata za Olubomba, Namanga na
Kimokoa na wanajiandaa na Kata za Kamwanga, Tingatinga, Olumorodi na
Sinya. Karatu wanaendelea na Usajili kwenye Kata ya Karatu na Rhotia
kabla ya kuhamia Ganako. Wilaya ya Ngorongoro wameanza na Tarafa ya
Ngorongoro kabla ya kuanza Mitijo.
Uongozi wa Mkoa umejizatiti
kuhakikisha wananchi wote wanasajiliwa kwa wakati na kupata Vitambulisho
vya Taifa vitakavyowawezesha kushiriki katika shughuli mbalimbali za
uzalishaji mali pamoja na upatikanaji kirahisi wa huduma za kijamii.
About Author

Advertisement

Related Posts
- FRIEDKIN CONSERVATION FUND WATOA MILLIONI 84 KUSAIDIA MIRADI YA MAENDELEO KWA JAMII YA MOYOWOSI, UVINZA NA UGALA02 Oct 20180
Baadhi ya wakurugenzi na viongozi wa Friedkin Conservation Fund wakiwa katika maonesho ya na...Read more »
- MOBISOL YASHIRIKI SIKU YA USAFI WA MAZINGIRA DUNIANI, WAHIMIZA MATUMIZI YA NISHATI JUA KUTUNZA MAZINGIRA17 Sep 20180
Baadhi ya wafanyakazi wa Mobisol Wakifanya usafi wa mazingira jijini Arusha mapema leo Baadhi ...Read more »
- JERRY MURRO ATOA MKWARA MZITO KWA WANAARUMERU MARA BAADA YA KUAPISHWA31 Jul 20180
Mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo katikati akiwa na wakuu wapya wa wilaya za Arumeru Bwana J...Read more »
- WAANDISHI WAWASILI KWA MGANGA WA JADI ILI KUMUELIMISHA JUU YA MADHARA YA UKEKETAJI KWA WATOTO WA KIKE.01 Jun 20180
Waandishi wa redio jamii tano Tanzania toka katika mikoa minne ya Arusha,Manyara,Dodoma na ...Read more »
- WAMAASAI, WASONJO WATAKIWA KUACHA UKEKETAJI01 Jun 20180
Jamii za Kimaasai na Sonjo zinazopatikana katika wilaya ya Ng...Read more »
- WADAU WA UTALII JIJINI ARUSHA WATOA MSAADA KUBORESHA HUDUMA YA AFYA31 May 20180
WADAU wa utalii mkoani Arusha wamekabidhi msaada wa Vitanda 40 kumi &nbs...Read more »
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.