PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: UPENDO FRIENDS YASAIDIA KITENGO MAALUM CHA WALEMAVU
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
Kaimu Afisa Elimu Shule ya Msingi wilaya ya Arusha mjini  Eunice Tondi akikabidhi sare za shule kwa Mwanafunzi wa Shule ya Msingi Meru ki...
Kaimu Afisa Elimu Shule ya Msingi wilaya ya Arusha mjini  Eunice Tondi akikabidhi sare za shule kwa Mwanafunzi wa Shule ya Msingi Meru kitengo Maalumu  zilizotolewa na Shule ya Msingi Upendo Friends Academy ,Kulia  ni .Picha na Ferdinand Shayo

Mkurugenzi wa shule ya Upendo Friends  Isabella Mwampamba (Watatu kulia)  akikabidhi msaada katika shule ya msingi Meru Kitengo Maalumu kilichopo wilaya ya Arusha Mjini.Picha na Ferdinand Shayo

Mkurugenzi wa shule ya Upendo Friends  Isabella Mwampamba akikabidhi msaada katika shule ya msingi Meru Kitengo Maalumu kilichopo wilaya ya Arusha Mjini.Picha na Ferdinand Shayo


Mkurugenzi wa shule ya Upendo Friends  Isabella Mwampamba   akikabidhi msaada katika shule ya msingi Meru Kitengo Maalumu kilichopo wilaya ya Arusha Mjini.Picha na Ferdinand Shayo


Mkurugenzi wa shule ya Upendo Friends  Isabella Mwampamba   akikabidhi msaada katika shule ya msingi Meru Kitengo Maalumu kilichopo wilaya ya Arusha Mjini.Picha na Ferdinand Shayo


Na Ferdinand Shayo,Arusha.

Shule ya Msingi ya Upendo Friends imesaidia kitengo Maalumu cha Watoto wenye mahitaji maalumu wakiwemo walemavu wasiosikia na kuona ikiwa ni njia mojawapo ya kuunga mkono juhudi za serekali katika kuboresha elimu kwa watoto wenye ulemavu.

Mkurugenzi Mkuu wa Shule hiyo Isabella Mwampamba alisema kuwa wamefika katika kitengo cha watoto wenye uhitaji maalumu kilichopo katika shule ya Msingi Meru na kutoa misaada ya chakula pamoja na vifaa vya michezo.

Isabella alisema kuwa ni wajibu wa wanajamii kuhakikisha kuwa wanawasaidia watoto wenye uhitaji kwa kuboresha mazingira ya kujifunzia na miundombinu rafiki kwa watoto wenye ulemavu.

Kaimu Afisa Elimu shule ya Msingi  Wilaya ya Arusha Mjini  Eunice Tondi  alisema kuwa serikali imeendelea kuwekeza kwenye elimu ya watoto wenye ulemavu kwa kuongeza vifaa vya kisasa kwa watoto wasiona ili waweze kufanya vizuri kitaaluma.

“Kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo serikali imeongeza nguvu na kuboresha vitengo vya watoto wenye ulemavu ili waweze kupata elimu bora na kujikwamua kimaisha “ Alisema

Mkuu wa Shule ya Msingi Meru Musa Luambano ameshukuru shule ya Upendo Friends kwa kujitolea kusaidia shule hiyo na kuhakikisha kuwa wanafunzi wanapata chakula ili waweze kuhudhuria darasani vizuri pia amezitaka shule nyingine binafsi kuelekeza nguvu katika kusaidia vitengo maalumu.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top