PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: Mbunge Awalilia Watoto Wanaofanyiwa Vitendo vya Unyanyasaji
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
    Mbunge wa Viti Maalumu wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala, Anatropia Theonest(Chadema) amesema watoto 244 wamefanyiw...



Mbunge Awalilia Watoto Wanaofanyiwa Vitendo vya Unyanyasaji
Mbunge wa Viti Maalumu wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala, Anatropia Theonest(Chadema) amesema watoto 244 wamefanyiwa vitendo vya unyanyasaji katika halmashauri hiyo kwa kipindi cha robo tatu ya mwaka huu.

Akizungumza leo, Agosti 13 Mbunge huyo amesema takwimu zilitolewa na Idara ya Ustawi wa jamii kwenye baraza la Madiwani zimeonyesha kati yao 85 walibakwa, 74 wakitelekezwa na 20 walilawitiwa.

Amesema matukio hayo yameongezeka kutoka 107 mwaka 2006 huku mtoto wa kike akiwa kwenye hatari ya kukosa haki ya elimu kutokana na kupata mimba.

"Ni lazima tusimame kwa pamoja tuweze kupaza sauti kwasababu tukiacha vitendo hivi viendelee tutajenga kizazi cha aina gani? cha walemavu?,"alisema

Aidha, amesema atawasilisha bungeni hoja binafsi ya kutaka marekebisho ya Sheria ya mwaka 1979 ili kuwapa haki watoto wanaopata mimba kupata haki ya kuendelea na masomo.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top