Dk. Jane akikabidhiwa cheti cha kutambua mchange wake kwa Tanzania kwa kuhifadhi Sokwe na wanayama wengine |
Home
»
»Unlabelled
» TANAPA YAMPATIA DKT. JANE GOODALL TUZO YA UTAFITI WA MIAKA 60 YA MAISHA YA SOKWE TANZANIA
Dkt.
Jane Goodal ambaye ni raia wa Uingereza alianza utafiti katika Hifadhi
ya Gombe mnamo miaka ya 60 akiwa na umri wa miaka 26.
Katika
utafiti wake amegundua mambo mengi ikiwemo jinsi Sokwe wanavyojitambua,
kuwa na hisia na jinsi wanavyoishi kwa ushirikiano kama walivyo
binadamu.
Akizungumza
katika hafla hiyo Dkt Goodal anasema wakati anaanza kufanya utafiti
ilikuwa vigumu Sokwe hao kumkaribia kwani walikuwa wanamuogopa na
ilikuwa ni mara ya kwanza kwao kumuona mtu mweupe, lakini alifanya
jitihada hadi wakamzoea na kuanza kumsogelea na kumuona mtu wao wa
karibu.
Anasema alitumia mbinu mbalimbali kama vile kuwapatia ndizi na vyakula vingine hadi wakamzoea.
Wakati
wa hafla hiyo iliyofanyika katika Chuo cha Utalii katikati ya jiji la
Dar es Salaam, viongozi na wageni waalikwa walipata wasaa wa kuangalia
picha mbalimbali za matukio ya sokwe wakiwa na Jane Goodall.
Katika
utafiti wake amefanikiwa kuanzisha chuo na kutunga vitabu pamoja na
video zinazoelezea maisha yake na Sokwe katika Hifadhi ya Gombe mkoani
Kigoma.
Katika
hafla hiyo walihudhuria Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne
Maghembe, Mwenyekiti wa Bodi ya Tanapa, Mkuu wa Majeshi mstaafu Jenerali
George Waitara, Mwanasiasa Mkongwe Getrude Mongela, Mwenyekiti wa Bodi
ya Chuo cha Goodall, Mhe. Lembeli pamoja na mabalozi mbalimbali na
waalikwa wengine. 
Waziri
wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe (kushoto) akimkabidhi
Dk. Jane Goodall tuzo maalumu kwa kutambua mchango wake wa utafiti wa
miaka 60 wa maisha ya Sokwe pamoja na uhifadhi wa wanyama wengine
kwenye hifadhi ya Gombe, mkoani Kigoma katika hafla iliyofanyika jijini
Dar es Salaam leo. Tuzo hiyo iliandaliwa na Mamlaka ya Hifadhi za Taifa
(Tanapa).
Jane akipatiwa pia zawadi ya kinyago cha Sokwe
Jane akikabidhiwa picha ya Sokwe
Mama Mongela akimvisha Jane zawadi ya vitenge
Dk Jane akitoa maelezo kuhusu maisha ya Sokwe
Waziri Maghembe akipata maelezo kuhusu maisha ya Sokwe yalivyo
Wasanii wa Tanapa wakitumbuiza kwa wimbo
Mwenyekiti
wa Bodi ya Tanapa, Mkuu wa Mjeshi Mstaafu, Jenerali Waitara akitoa
shukrani nyingi kwa Dk Jane kwa kazi kubwa aliyoifanya na kuiletea
Tanzania sifa lukuki duniani
Wageni
waalikwa wakisikiliza kwa makini wakati Waziri Maghembe akihutubia
katika hafla hiyo, ambapo alisema kuwa Dk. Jane ambaye wakati anaaza
utafiti yeye alikuwa darasa la pili, lakini utafiti wake umeiletea sifa
kubwa Tanzania na utakuwa ni urithi wa kipekee maishani
Wageni waalikwa wakisikiliza kwa makini
Profesa Magembe akihutubia katika hafla hiyo ya kumpatia tuzo Dk. Jane
Baadhi ya mabalozi waliohudhuria hafla hiyo
Dk Jane akielezea historia yake na jinsi alivyofanikiwa kufanya utafiti huo wa sokwe
Lembeli akitoa neno la shukrani
Jane akiwa katika picha ya pamoja na mabalozi waliohudhuria hafla yake pamoaja na viongozi mbalimbali
Jane akiwa katika picha ya pamoja na wanahabari baada hafla kumalizika
About Author

Advertisement

Recent Posts
- The Maasai Families in Longido District allegedly use baptism ceremonies to conceal FGM practices17 Sep 20240
By our Reporter in Longido Some Maasai families in Longido District, Arusha Region ar...Read more »
- Tanzanian Shillings 6.56 Trillion Investment in the JNHPP Project Bears Fruits for the Nation14 Sep 20240
By Our ReporterThe Public Investments Committee (PIC) of Parliament visited the construction site of...Read more »
- 35 teams set to battle in Chem Chem Cup 2024: Sh78 million up for grabs10 Sep 20240
By Mussa Juma, MaipacBabati. A total of 35 teams will participate in the 2024 Chem Chem Cup, costin...Read more »
- Mwiba holdings Donates house for Health Workers and 194 bicycles to Meatu students.29 Aug 20240
By Our Staff Writer in MeatuMwiba Holdings Ltd, a tourism and conservation investment company ...Read more »
- Mount Kilimanjaro porters' jobs in jeopardy due to foreign influence and controversial practices29 Aug 20240
KPAP's influence has shifted the tourism market, with foreign agents favoring their affiliates over ...Read more »
- Tanzania ramps up health education amid Mpox threat25 Aug 20240
By Staff WriterIn a bold move to safeguard Tanzania from the looming threat of Mpox, the Ministry o...Read more »
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.