PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: WAJASIRIAMALI WATAKIWA KUJIKITA KATIKA UFUGAJI KUKU
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
Mjasiriamali  na Mfugaji wa Kuku Boniventura Shiyo akiwalisha kuku anaowafuga,ni miongoni na watu wanaonufaika kiuchumi kutokana na...


Mjasiriamali  na Mfugaji wa Kuku Boniventura Shiyo akiwalisha kuku anaowafuga,ni miongoni na watu wanaonufaika kiuchumi kutokana na biashara hiyo.Picha na Ferdinand Shayo


Na Ferdinand Shayo,Arusha.

Wajasiriamali nchini wametakiwa kujikita katika Ufugaji wa kuku wa Kienyeji na kisasa ili waweze kunufaika kiuchumi kufuatia ongezeko la uhitaji mkubwa wa mayai na nyama katika maeneo ya mengi hususan kwa wafanyabiashara wa vyakula.

Hayo yameelezwa na Mjasiriamali Boniventura Shiyo anayejihusisha na ufugaji huo amesema kuwa kwa sasa biashara hiyo imemuongezea kipato ambacho anakitumia kujiletea maendeleo pamoja na kuendesha familia pasipo kuyumba.

Mjasiriamali huyo amewataka Watanzania kujenga tabia ya uthubutu kwani soko la biashara ya kuku ni kubwa na linazidi kukua kila kukicha.

Hata hivyo Boniventura amesema kuwa kwa sasa anatumuia mashine maalumu ya inayototoa mayai na kuwa vifaranga maarufu kama incubator ambayo imemuongezea fursa ya kuwa muuzaji wa vifaranga pia.

Biashara ya ufugaji wa kuku ni moja kati ya biashara zinazoshamiri kwa kasi katika maeneo mingi nchini hususan maeneo ya mijini ambapo ndipo masoko makubwa yanapatikana kutokana na idadi kubwa ya watumiaji wa bidhaa za mayai na nyama ya kuku.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top