PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: Degree/Diploma si kazi; Sehemu ya pili
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
Ni kweli kabisa, kuna watu wengi walio na kazi lakini hawana Elimu, Leo hii si jambo la kushangaa kuona kampuni kubwa ina H...

https://lh6.googleusercontent.com/-xIpjgqv2UcA/AAAAAAAAAAI/AAAAAAAAAAA/F_1A0MyWG1s/s128-c-k/photo.jpg

Ni kweli kabisa, kuna watu wengi walio na kazi lakini hawana Elimu, Leo hii si jambo la kushangaa kuona kampuni kubwa ina HR wa kike aliyeishia form four lakini secretary wake ni diploma. Juzi tu tumeona Waziri akiwa na diploma lakini wasaidiz wake wana PhD.
Hata wazazi wetu walifanya kazi mbalimbali za mikono na kisha kutusomesha, wengine humu wamesomeshwa na maziwa tu, wengine kahawa, wengine, mbao, wengine viazi, wengine sukari. Wazazi hawa hata siku moja hawakusema 'ETI HATUNA KAZI' na kukaa kuilalamikia serikali, BADALA YAKE WALIKAZANA NA KAZI ZAO ZA MIKONO in fact walijua hawawezi pata KAZI za ajira kwa kuwa hawakusoma. Siku hizi hata mlinzi lazima uwe form four na cheti cha mgambo.
Mfumo wa Elimu Tanzania hasa elimu isiyo ya ufundi au udaktari, hauandai 'KAZI' unaandaa 'AJIRA' na hapa ndio penye tatizo, kwa kuwa unapomaliza Chuo na degree/diploma ya sociology, habari, ualim nk jamii inakutegemea uwe na kazi ya ajira au ya kujiajiri. But ukiingia mtaani kuna watu kibao wanaohitaji ushauri wa kijamii, kindoa, kisheria na kidini, KOSA UNALOFANYA UNASOMA TU sociology vitabuni bila kujiongeza. UKIMALIZA CHUO unajikuta huna ujuzi wowote wa kupata kazi ya ajira au kujiajiri.
Hata waliosoma masomo ya biashara hujikuta hawawezi hata kuandika mpango wa biashara wa Kuku. Hawa walisomo ili kuajiriwa ktk kampuni za wengine.
Na hapa ndipo thamani halisi ya degree yako inapojulikana.
Mfumo huu mbovu umerithishwa toka wakoloni, na imekuwa ngumu kubadilika.
Unaposikia mtoto wa miaka 10 Finland amegundua tatizo ktk mtandao wa kijamii wa Facebook usidhanie ni kitu cha kubahatisha, mfumo wa shule unamruhusu kuwa curious.
SASA HIVI UPO SHULE MATHALANI HUONI TOFAUTI SANA. LAKINI UKISHAMALIZA SHULE NDIO UTAANZA KUONA TOFAUTI NA KUJIULIZA THAMAN YA DEGREE/DIPLOMA YANGU IPO WAPI.
Binafsi huwa napingana sana na wanaoilaumu serikali kwa kukosa kazi kwao, huwa nawauliza. JE FURSA HAKUNA?
KAMA ZIPO KWA NINI MIMI NIPATE WEWE UKOSE?
Na ndio mada ya Leo
Katika mahali ulipo
''JE FURSA ZIPO AU HAZIPO NA KAMA ZIPO JE UNAWEZA ZIPATA''?
Chagua linalokufaa
A. Fursa Zipo na naweza zipata
B. Fursa zipo but zinavipingamizi
C. Fursa Hazipo
D. Sijui
Chagua jibu moja TU!
Na....Mr.Adson Kagiye


About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top