PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: MAKALA YA UCHUMI: ANZA UPYA LEO UFANIKIWE
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
Kushoto ni mfanyabiashara katika soko la Morombo jijini Arusha Bi. Neema Mushi akimuelezea mwadishi wa habari kulia Bw.Samson Festo hali...
Kushoto ni mfanyabiashara katika soko la Morombo jijini Arusha Bi. Neema Mushi akimuelezea mwadishi wa habari kulia Bw.Samson Festo hali halisi ya biashara inavyokwenda tangu mwezi januari  ambapo biashara kwa sasa imekuwa ngumu sana kwao hali inayowalazimisha kushusha bei ya bidhaa ili mzigo uende ili kuepusha mzigo kuwaharibikia . PICHA NA HAPPINESS CHARLES,NMG.

Na Ferdinand Shayo,Arusha.

Haijalishi umepitia magumu mangapi,mateso na manyanyaso,haijalishi umekataliwa mara ngapi ,haijalishi umekatishwa tama mara ngapi,haijalishi umeanguka mara ngapi chamsingi nyanyuka endelea kukaza mwendo kuyaelekea mafanikio yako.

Inawezekana historia yako inakurudisha nyuma nataka nikuambie kwamba Historia yako haina nguvu kama maono uliyonayo ,kama mawazo mazuri uliyo nayo wala haifikii ndoto ulizonazo.

Naamini kuwa maisha yako yanaweza kubadilika ukiamua sasa,historia yako inaweza kubadilika ukiamua sasa ,kutoka kuwa masikini wa kutupwa kuwa tajiri wa kutisha ,kutoka kuwa mtu wa kudharaulika  hadi kuwa mtu wa kuheshimika sana ,nguvu ya kubadilika iko ndani yako chamsingi uamue.

Mafanikio ni kuchagua  sio bahati ama majaliwa kama wengi wanavyofikiri,chagua unataka kuwa nani,unataka kuwa na uchumi wa namna gani,unataka kuwa na familia ya namna gani,watoto wa namna gani,unataka kuwa nani kwenye jamii yako,taifa na dunia.

Amua sasa kubadilika uishangaze dunia ,udhihirishe Ukuu wako Mungu aliokuumbia ,hujazaliwa kuwa mtu wa chini usiridhike na hali uliyonayo.

Uishi maisha unayoyataka usiishi maisha yoyote,jua unataka nini katika haya maisha ,maana kama hujui unataka nini chochote kinaweza kukufaa.

Wewe si mtu wa chochote ,wewe ni Mkuu sana ,wewe ni wa kipekee sana,wewe ni wa tofauti sana usikubali kuishi maisha ya kawaida,uchumi wa kawaida,maisha ya kawaida ,familia ya kawaida .
Lazima utoke huko uelekee kwenye Ukuu wako  (your Greatness) hapa siongelei maisha unayoyatamani kuishi bali naongelea maisha unayostahili kuishi maana kama Mungu amekupangia uishi kiwango cha juu ukaishi kiwango cha chini sio sawa.

Huu ni mwaka wa kwenda kwenye viwango vingine vya uchumi,elimu,kiroho usikubali kuwa Yule Yule miaka nenda rudi,unastahili zaidi ya hapo.

Rafiki yangu Godrich Izack huwa ananiambia unastahili zaidi ya hapo maana yake usiishie hapo  ulipo kuna kiwango kingine kikubwa zaidi ambacho unapaswa uwe usiishie hapo ulipo.

Tabia ya kuridhika maisha ya chini au ya wastani ulionayo ni tabia mbaya sana inawakwamisha watu wengi kufikia pale ambapo wanatakiwa wafike.

Watu wengi duniani wanaishi maisha yaliyopo wachache sana wanaishi maisha wanayoyataka na hilo ni tatizo kubwa  watu wafanya kazi ambazo hawazitaki ,hawazipendi wanafanya tu kwasababu zinawaingizia fedha  ya kuishi,wameoa ama kuolewa na watu ambao hawawataki ,wanaishi nyumba ambazo hawazitaki  na maisha yao  yamejaa utumwa ,fedheha,uchungu na maumivu.

Tatizo sio wao tatizo ni maamuzi yao kwasababu maisha ni matunda ya maamuzi yako unayoyafanya leo matokeo yake ni kesho yako.

Maamuzi yako yana nguvu kubwa ya kubadilisha maisha yako,amua sasa .

0765938008

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top