Mbunge wa Ubungo, Saed Kubenea (44) amekana kumtukana Mkuu wa wilaya ya
Kinondoni, Paul Makonda tarehe 14 Desemba 2015 walipokutana katika
Kiwanda cha Tooku Garments Co. Ltd. kilichopo eneo la External Mabibo
kwa madhumuni ya kutatua mgogoro kati ya wafanyakazi na uongozi wa
kiwanda hicho
Katika kesi inayosikilizwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Kisutu,
Wakili wa Serikali mwandamizi, Kishenyi Mutalemwa alimsomea mshtakiwa
maelezo ya kesi hiyo ambapo baadhi ya mashtakiwa aliyakana.
Akisomewa maelezo ya kesi, Saed Kubenea alikiri kuwa ni mbunge wa Ubungo
na pia alikiri kuwa anamfahamu mlalamikaji katika kesi hiyo kuwa ni
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Makonda na kwamba ni kweli kuwa tarehe 14
Desemba 2015 alifika katika Kiwanda cha Tooku Garments Co. Ltd
kulikokuwa na mgomo wa wafanyakazi.
Hata hivyo, alipoelezwa kuwa anashtakiwa kwa kosa la kumtolea lugha
chafu Makonda ambapo alimwita kuwa ni kibaka, mpumbavu, mjinga na cheo
chake ni cha kupewa kitendo ambacho kingeweza kusababisha uvunjifu wa
amani na utulivu; Saed Kubenea alikana.
Kufuatia Kubenea kukana mashitaka yanayomkabili, Hakimu mkazi mkuu wa
mahakama hiyo , Thomas Simba alisema mashahidi sita wa upande wa
mashtaka wataanza kutoa ushahidi wao Januari 20 na 21, 2016 katika
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.
About Author

Advertisement

Related Posts
- JENGO LA MAMLAKA YA HIFADHI YA NGORONGORO KUWA KIVUTIO CHA KIHISTORIA CHA UTOAJI WA HUDUMA ZA UTALII JIJINI ARUSHA10 Apr 20180
Na Hamza Temba - WMU........................................................JENGO la kit...Read more »
- Maalim Seif Amjia Juu Msajili Sakata la Kufukuzwa Uanachama Wanachama Saba wa CUF19 Aug 20170
Katibu Mkuu wa CUF Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad amemjibu Msajili wa...Read more »
- Tume ya Taifa ya Uchaguzi(NEC) imewateua 8 kuwa Wabunge wa Viti Maalum CUF27 Jul 20170
Kwa mujibu wa Ibara ya 78(4) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzan...Read more »
- Baada ya Jecha Kudai Alikuwa Sahii Kufuta Uchaguzi ZNZ,Maalim Seif Aibuka na Haya..!!!24 Jan 20170
Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad amesema ameshamalizana na mwenyekiti wa Tume y...Read more »
- Sumaye - Sishtushwi na Utendaji Kazi wa Magufuli Kwani Anatekeleza Ilani ya Chadema16 Jan 20170
WAKATI Rais wa Awamu ya Tano, John Magufuli akitekeleza masuala...Read more »
- Kikwete Atoa Dongo "Wapo Watu Walidhani CCM ingekufa na Walishajiandaa na Salamu za Rambirambi"22 Jul 20160
MWENYEKITI wa Taifa wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais mstaafu Jakaya Kikwete, a...Read more »
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.