PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: JKT OLJORO YAENDELEA KUGAWA DOZI LIGI DARAJA LA KWANZA.
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
NA; YOHANA CHALLE. ARUSHA. MAAFANDE    Wa timu ya JKT Oljoro ya jijini Arusha Mwishoni mwa wiki wameendelea    kugawa dozi kwa timu...
NA; YOHANA CHALLE.
ARUSHA.

MAAFANDE  Wa timu ya JKT Oljoro ya jijini Arusha Mwishoni mwa wiki wameendelea  kugawa dozi kwa timu pinzani baada ya kufanikiwa kuwalaza timu ya Geita Gold Sports ya mkoani Geita kwa jumla ya mabao 2-1 katika  mchezo uliopigwa ndani ya dimba la sheikh Amri Abeid jijini Arusha.

Baada ya Ushindi huo timu hiyo ya Oljoro imefikisha jumla ya pointi 11 na kushika usukani wa kundi hilo sawa na wapinzani wao Geita Gold Sport huku zikitofautiana mabao ya kufunga na kufungwa.

Swalehe Hussein aliweza kuiandikia timu yake ya Jkt Oljoro Bao la kuongoza dakika ya  17  kwa njia ya kichwa , baada ya kupokea mpira wa kurushwa kutoka kwa  Yusuph Machogote, Bao lilidumu kipindi chote cha dakka 45 za kipindi cha kwanza.

JKT Oljoro waliingia kipindi cha pili wakiwa na  malengo  ya kufunga mabao zaidi,huku ikiwachukua dakika moja tangu watoke mapumziko kuandika bao la pili lililofungwa  na  Lucas Charles  dakika ya 46  na timu ya Geita Gold Sports ilijipatia bao lake la kufutia machozi lililowekwa nyavuni na  mchezaji Hillary Bingwa.

Akizungumza mara baada ya pambano hilo kocha msaidizi wa timu ya JKT Oljoro Joely Mwambegele alisema kuwa timu yao itahakikisha inamaliza raundi hii ya kwanza ikiwa inaongoza kundi hilo  kwani wanataka waweze kushiriki ligi kuu msimu ujao ambapo aliwaomba wakazi wa Arusha kuendelea kuwaunga mkono zaidi.

Kwa upande wake kocha msaidizi wa timu ya Geita Gold Sports , Teru Yusuph alieleza kuwa mchezo ulikuwa mzuri  na timu yake imeweza kucheza mpira vyema.

“Bahati ya kuibuka na ushindi haikuwa ya kwao na tutajipanga zaidi kwa michezo ijayo kwa ligi bado inaendele na tuna nafasi ya kulejesha matumaini yetu kwa wapenzi wetu” alisema Yusuph.

Mchezo mwingine wa ligi daraja la kwanza ulichezwa katika uwanja wa Ushirika Mjini Moshi ,Mkoani Kilimanjaro ambapo ulimalizika kwa wenyeji  Timu ya Panone Fc kuibuka kidedea kwa ushindi mwembamba wa bao 1-0 ,Dhidi ya timu ya Polisi Mara.

Timu ya JKT Oljoro itashuka tena uwanjani jumamosi ijayo ambapo itawakaribisha maafande wenzao wa Timu ya Polisi Tabora  huku timu ya Panone FC ya Mkoani Kilimanjaro itakuwa ikicheza katika uwanja wao wa nyumbani na timu ya Rhino Rangers ya mjini Tabora.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top