PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: JKT OLJORO KUBADILI KIKOSI CHAKE DIRISHA DOGO.
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
NA; YOHANA CHALLE. ARUSHA. Kocha Mkuu wa JKT Oljoro Ally Mohamedi amesema kuwa watahakikisha wanabadili kikosi cha timu hiyo...



NA; YOHANA CHALLE.
ARUSHA.

Kocha Mkuu wa JKT Oljoro Ally Mohamedi amesema kuwa watahakikisha wanabadili kikosi cha timu hiyo pindi dirisha dogo la usajili litakapofunguliwa Septemba 15.

Kocha huyo alisema haya mwishoni mwa wiki baada ya mchezo Katika mwendelezo wa Ligi daraja la kwanza (FDL) dhidi ya Poloisi Tabora jijini hapa ambapo katika mchezo huo Oljoro walishinda bao 1-0.

Mchezo huo ulikuwa wa kuhitimisha mzunguko wa kwanza wa ligi daraja la Kwanza (FDL), ulichezwa katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid Jijini hapa, na kushuhudiwa na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Bodi ya ligi Boniface Wambura.

Oljoro imefanikiwa kubaki kileleni ikijikusanyia alama 14 na kuiacha Polisi Tabora ikiwa na alama 11 timu ambayo ilikuwa inakimbizana na Oljoro Kileleni.

katika mchezo huo Polisi walionekana kuwamudu wenyeji wao kwa kipindi chote cha dakika 45 za kipindi cha kwanza kabla ya Swalehe Iddi kwafungia Oljoro Bao pekee na la ushindi mnamo dakika ya 61 baada ya kupokea pande safi kutoka kwa Paulo Malipesa.

Kocha Mkuu wa Oljoro Ally Mohamedi maarufu kama Babu Kidi alizungumza kwa mara ya kwa mna waandishi wa habari tangu atue kwenye timu hiyo na kusema kuwa mara baada ya kumalizika mzunguko huo kilichobaki ni kukiimalisha zaidi kikosi chake.

"Nimefurahishwa wachezaji wangu wamebadilika na wanajitua kwa kuwa wameshafahamu kuwa wanahitaji kupanda daraja kucheza ligi kuu msimu ujao hivyo kila mchezaji acheza kwa lengo moja tu tulilojiwekea la kupanda ligi kuu" alisea Mohamedi

Aliongeza kuwa watahakikisha wanaongeza nguvu pindi dirisha Dogo la usajili litakapo funguliwa Septemba 15 na kufanya timu inabaki kileleni hadi mwisho wa FDL.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top