PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: VIKUNDI VYA VICOBA NI SULUHISHO KWA WAJASIRIAMALI.
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
NA; YOHANA CHALLE. PRINCEMEDIATZ Kila mtu anandoto ya kuwa tajiri, maana hakuna anayependa umasikini, kwasababu mtu masikini hata...

NA; YOHANA CHALLE. PRINCEMEDIATZ


Kila mtu anandoto ya kuwa tajiri, maana hakuna anayependa umasikini, kwasababu mtu masikini hata akiwa na mawazo mazuri hawezi kusikilizwa,na wakati mwingine hata heshima yake hushushwa na yule tajiri huheshimiwa sana hata kama kwao ni mdogo na hata kama hakuenda shule hilo halijalishi.

Akina mama wengi ndio wanaonekana kujikusanya pamoja na kuunda vikundi vidogovidogo vya ujasiliamali kwa ajili ya kujikwamua kimaisha ya hali ya chini na kufikia angalau watu wa hali ya kati,huku wakina baba wakionekana kwa mbali sana.

Shirika lilsilo la kiserikali la Usariver Community Organization (URICO), lililopo wilayani Arumeru Mkoani hapa ambalo linashuhulika na shughuli mbalimabli ikiwemo kulea watoto yatima, kwa kutambua umuhimu wa vicoba imeamua kuvikuasanya pamoja vikundi mbalilmbali katika wilaya hiyo.

Katibu mkuu wa URICO Daud Lezile alisema kuwa kwa kutambua umuhimu wa akinamama katika jamii walivikusanya vikundi takribani 23 vilivyopo ndani ya wilaya hiyo ili kuwaweka pamoja na hatimaye kuwa na kundi moja lenye nguvu.

“katika vikundi tulivyo vikutanisha hapo awali vilikuwa 23 na vyote viliitikia wito, lakini vikundi 12 tu ndivyo vilivyokubali kuungana na sisi ni kama wasimamizi wao katika kufanikisha yale waliyolenga kuyafanikisha” alisema Lezile

URICO inawasaidia wajasiliamali kupata elimu mbalimbali ikiwemo ya biashara ndogondogo (kuuza mchele na mboga mboga na chakula), kilimo cha mpunga, mahindi na mboga mboga ufugaji (ng’ombe, mbuzi na kuku na bata) 

Shirika hilo limefanya juhudi za kuwaunganisha wanavikoba na hatimaye kuwa kikundi kimoja kijulikanacho kama Muungano wa Vicoba Usaiver (MUVIU), ambapo kikundi kinawasaidia kupata mikopo katika taasisi za kifedha.

Licha ya kupata mikopo MUVIU inasaidia wajasliamali kubadilishana mawazo na kuelezea uzoefu walionao baadhi ya watu mbalimbali,kuendesha,kuinua, kushawishi,kuboresha hali na ustawi wa kiuchumi na jamii ya wanachama wake.

“mtandao huu utakuwa ni kiungo kati ya vikundi vipya na vya zamani ili waweze kuboresha shughuli zao za ujasiliamali,kujenga uwezo wa elimu ya ujasiliamali kwa wanachama, kujenga sekta binafsi na za serikali” alisema Lezile

Aliongeza kuwa vikundi vya ujasiliamali ni vizuri sana kwasababu hata mashirika, serikali, na wafadhili huangalia sehemu za namna hiyo katika kutoa mitaji na sio kwa mtu moja mmoja.

Vikundi vingi vimekua vikiishia njiani kutokana na wajasiliamalin wengi kutokuwa na elimu ya kutosha ya kuendeleza mitaji yao kwenye biasha kwasababu kila biashara lazima kuwepo na elimu juu ya uendeshwaji wa biashara hiyo.

kutoaminiana kati ya wanavikundi kutokana na wachache kujiona kama kikundi ni halali yao na kutaka kujimilikisha, kwakutokuwa na uaminifu, pia kushindwa kusimamia vizuri miladi yao hata kama wanamtaji wa kutosha.

Elimu nyingi tumeona zinatangazwa juu ya elimu ya ujasiliama kutokana na kuamini kuwa mjasiliamali hataweza kuendesha biashara yake asipo kuwa na elimu itakayo mwezesha katika kufanikisha lengo lake

Suala la ajira kwa nchi yetu ni tatizo kubwa hasa vijana wanaomaliza elimu zao wakitegemea kupata ajira serikalini au katika mashirika mbalimbali na hatimaye kujikuta wakizunguka na bahasha miaka mingi bila mafanikio.

Vijana mara nyingi wanailaumu serikali kwa kushindwa kutengeneza mifereji ya ajira kwao, huku serikali kupitia wizara ya ajira ikitoa majibu kadha wa kadha.

Njia pekee ambayo vijana wanahashwa kufanya katka kutekeleza malengo yao ni kujiajiri kutoikana na elimu ya ujasiliamali wanayoipata na sio kutegemea kuajiriwa.

Japo ushauri huo vijana hawaukubali kwasababu ya kudai watajiajiri vipi wakati hawana mitaji?, serikiali haiwapi nafasi, vijana hawaaminiki na hata hivyo vijana hawathaminiwei katika taifa lao.

Licha ya faida zote hizo juu ya elimu ya ujasiliamali hukisaidia kikundi cha URICO kuwa wabunifu katika kuanzisha biashara mpya maeneo ambayo bado bidhaa zao hazijafika na tayari kuna wateja.

Mipango ya biasha kwa siku za usoni ili kupanua soko lao na kuweza kupambana katika soko la biashara kwa kuwafikia wateja walipo na kutoa huduma nzuri na safi ili kuweza kuongeza uaminifu wao na kushinda ushindani juu ya vikundi vingine.

Mtaji ni kitu chochote ambacho unaweza kutumia katika kuzalisha kitu kingine kwa lengo la kupata faida,biashara yoyote lazima ianze na mtaji. Mtaji wa fedha au yeye mwenyewe mjasiliamali anaweza kuwa mtaji mfano kwa ujuzi, elimu na kufanya kazi kwa bidii.

Wajasiliamali wengi wanapata changamoto kubwa katika kupata mitaji ya kuanzishia biashara. Ni vigumu kuanzisha biashara bila kuwa na mtaji wa kutosha,hivyo basi mtaji ni muhimu sana lakini mtaji pekee hautoshi kuanzisha biashara.

Ni lazima uwe na elimu ya ujasiliamali ili uweze kufanikiwa katika biashara. kuna njia mbalimbali za kupata mtaji na njia hizo ambayo ni vyanzo vya ndani au vyanzo vya nje mfano  Mtaji   toka kwa mjasiliamali mwenyewe.

Huu ni mtaji ambao mjasiliamali anakuwanao kabla hajaanza biashara. huu ni mtaji bora sana kwani humilikiwa na mjasiliamali mwenyewe na hatakiwi kurudisha rejesho hata baada ya kupata faida.

Pia Mtaji ambao unapatikana wakati biashara inajiendesha ni faida inayopatikana katika biashara inaweza kutumika kama mtaji,njia hii ndio huchangia kukua kwa biashara.

Mkopo toka benki, huu ni mkopo ambao ulipaji wake ni wa muda mrefu,viwango vya riba si vikubwa sana ambavyo mjasiliamali anaweza kumudu kulipa endapo biashara itafanikiwa, mikopo ya benki inahitaji dhamana ya vitu visivyo hamishika mfano nyumba, shamba nk.

Elimu ya ujasiliamali kwa mjasiliamali ni muhimu sana, kutokana na changamoto wa ubunifu wa biashara. 

Nawakumbusha tu, yawezekana mlijisahau                                              0762801099 / 0652 362138

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top