PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: ZAIDI YA MASKINI MILION 3 WASAIDIWA NA TASAF MIKOA YA ARUSHA NA NJOMBE
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
Mussa Juma, Arusha. MFUKO wa Maendeleo ya jamii(TASAF) leo umezindua mradi wa kupunguza umasikini kwa watu milioni 3.1 kutoka halmas...

Mussa Juma, Arusha.

MFUKO wa Maendeleo ya jamii(TASAF) leo umezindua mradi wa kupunguza umasikini kwa watu milioni 3.1 kutoka halmashauri 14 za mikoa ya Arusha na Njombe unaogharimu kiasi cha dola 16.4 milioni ambazo ni zaidi ya Tsh 30 bilioni.
Mkuu wa mkoa wa Arusha, Felix Ntibenda akizindua mradi huo ambao ni sehemu ya mradi wa tatu wa kupunguza umasikini nchini, alisema wananchi 3.1 milioni watanufaika katika kupata maji safi,huduma bora za afya na elimu.
“katika awamu hii, TASAF inalenga kuondoa mapungufu katika huduma muhimu za kijamii,ikiwepo kusaidia jamii kutekeleza miradi ya umwagiliaji na shughuli za kuongeza kipato”alisema
Ntibenda alizitaja halmashauri ambazo zipo katika mradi huo kuwa ni Jiji la Arusha,halmashauri ya Monduli,Ngorongoro, Longido,Meru na halmashauri ya Karatu.
Alisema kwa mkoa wa Njombe, halmashauri ambazo zitagushwa ni Ludewa,Makete,Njombe,halmashauri Wanging’ombe,halmashauri za miji ya makambako na halmashauri ya Njombe.
Awali,Mkurugenzi mkuu wa TASAF , Ladislaus Mwamanga alisema fedha za kutekeleza miradi hiyo, zimetolewa na umoja wa nchi za wazalishaji wa mafuta (OPEC) ambapo awamu kwanza Ililenga mikoa ya Mtwara na Lindi ambapo kiasi cha dola milioni 10 zilitumika.
Alisema awamu pili ya mradi huo, pia ilitumika mikoa ya Mtwara na lindi ambapo kiasi cha Dola milioni 12 zilitumika na kuweza kuwa na mafanikio makubwa kutokana na kufanikisha miradi kadhaa ya maendeleo na kuchochea maendeleo.
Mwenyekiti wa halmashauri ya Karatu, Lazaro Maasai alieleza kuridhishwa na TASAF kuichaguwa halmashauri ya Karatu kuwa ni miongoni mwa halmashauri 14 ambazo zitanufaika na mradi wa TASAF awamu ya tatu.
Lazaro alisema anauhakika halmashauri yake na halmashauri nyingine zilizopata mradi huu, zitaweza kuchangia kuondoa matatizo mbali mbali ya kijamii na hivyo kuinua hali za maisha ya wananchi ili lengo la TASAF lifikiwe.
mwisho
CREDIT: SAUTI YA MNYONGE

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top