PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: maonesho ya biashara ya Uturuki na Tanzania yavuta wengi
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
MAONYESHO ya biashara ya bidhaa za Uturuki na Tanzania yaliyofanyika jijini Dar es Salaam kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee, yamevut...
MAONYESHO ya biashara ya bidhaa za Uturuki na Tanzania yaliyofanyika jijini Dar es Salaam kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee, yamevuta watazamaji wengi kuwa na shauku ya kutembelea mabanda mbali mbali likiwemo banda la Kampuni ya Jamii Media iliyoshiriki maonyesho hayo, ambao ni wamiliki wa mitandao maarufu ya mijadala kwa jamii kupitia mitandao ya kijamii, JamiiForums na FikraPevu nchini Tanzania.
Maonyesho hayo ambayo yalifanyika kwa siku tatu katika ukumbi huo na kumalizika leo, mbali na wananchi kujionea bidhaa mbalimbali kutoka kwa wafanyabiashara kutoka ndani na nje ya nchi baadhi yao wamejisajili na kuwa wanachama hai katika mtandao wa Jamii Forums ili kupata faida katika nyanja tofauti/mchanganyiko.
Aidha, baadhi ya wananchi walio wengi waliotembelea maonyesho hayo walipa fursa ya kujua namna Jamii Media inavyofanya kazi pamoja na manufaa yaliyopo kwa kutumia mitandao ya kijamii ikiwemo JamiiForums na FikraPevu.
Maonyesho hayo yalifunguliwa na Mwenyekiti wa Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF), Dk. Reginald Mengi,Mei 15, 2014 ambapo aliwataka watanzania kupitia maonyesho hayo kujijifunza kutengeneza bidhaa zenye ubora wa hali ya juu na zenye bei nafuu kama zilivyo bidhaa zinazotoka nchini Uturuki.
Dk. Mengi, aliwataka wawekezaji wa nje ya nchi kuja kuwekeza Tanzania ili Watanzania wajifunze teknolojia ya viwanda na kuongeza nafasi za ajira kukuza uchumi, pamoja na makampuni ya Kitanzania kushiriki maonyesho mbalimbali kama hayo kwani yatawasaidia kutafuta soko la bidhaa zao kwenda nje ya nchi na pia yatawapa nafasi ya kushiriki katika maonyesho kwenye nchi nyingine.
Mtandao wa JamiiForums unatajwa kuwa miongoni mwa mitandao ya kijamii inayosimamia uhuru wa habari, kuhabarisha na kushirikisha wananchi kwa habari na matukio katika kila nyanja. Husomwa na watu zaidi ya laki tatu hadi nne kwa siku na hivyo kuchangia kusambaza habari kwa haraka na upana kuliko chombo chochote cha mitandao ya Kijamii nchini.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top