UN yaripoti uovu Sudan Kusini
Umoja wa Mataifa umesema mapigano yenye sura ya kikabila yaliyozuka katikati ya Desemba mwaka jana Sudan Kusini yamesababisha mauaji ya kikatili na unyanyasaji dhidi ya maelfu ya raia na kampeni ya kukashifu umoja huo.
Mkuu wa shughuli za kusimamia amani wa Umoja wa Mataifa Herve Ladsous ameliambia baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuwa pamoja na makubaliano ya kusitisha mapigano ya Januari 23, lakini jeshi tiifu kwa rais Salva Kiir na wapiganaji waasi wanaoongozwa na makamo wa rais wa zamani alieondolewa madarakani Riek Machar wameendelea na harakati zao za kijeshi na kuyapa kisogo mazungumzo muhimu ya kisiasa kwa lengo la kupatikana suluhisho la mgogoro huo.
Kuzuka mapigano
Wapiganaji waasi katika baadhi ya miji
Mapigano Sudan Kusini yalizuka Desemba 15 miongoni mwa kikosi cha jeshi cha ulinzi wa rais mjini Juba, ambapo kwa kasi yakasambaa katika maeneo tofauti ya nchi hiyo na kuchukua sura ya mwelekeo wa mapigano ya kikabila kati ya kabila la Dinka, lenye kumuunga mkono rais Kiir na Nuer lenye utiii kwa Machar.
Afisa huyo mwandamizi wa Umoja wa Mataifa, Ladsous amesema mgawiko wa kisiasa umesababisha mgogoro kwa hivi sasa kwa kuathiri maisha ya kila mtu mmoja mmoja pamoja na utendaji wa serikali ya Sudan Kusini na taifa lenyewe kwa ujumla. Amesema ripoti ya uchunguzi ya awali inaonesha mauwaji pamoja na ukiukwaji mbaya sana haki za binaadamu umetekelezwa na pande zote zinazohasimiana katika mgogoro huo.
Post a Comment