PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: MAKAMU WA RAIS Dr. MPANGO KUSHUHUDIA MIAKA HAMSINI YA HIFADHI YA MLIMA KILIMANJARO
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
MLIMA KILIMANJARO   Na: Mwandishi wetu, Arusha  Makamu wa Rais dkt Philip Mpango anatarajiwa kushuhudia hifadhi ya Mlima Kilimanjaro ikitimi...

MLIMA KILIMANJARO 

 Na: Mwandishi wetu, Arusha 

Makamu wa Rais dkt Philip Mpango anatarajiwa kushuhudia hifadhi ya Mlima Kilimanjaro ikitimiza miaka hamsini tangu kuanzishwa kwake march 16 Mwaka huu.


Naibu Kamishna wa Uhifadhi na maendeleo ya biashara,Herman Batiho aneyasema hayo alipokuwa akitoa taarifa kwa waandishi wa habari makao makuu ya hifadhi za Taifa TANAPA Jijini Arusha mapema Leo.



"Kilele cha Mlima kilimanjaro kitafanyika Marangu Mkoani Kilimanjaro yalipo makao makuu ya Mlima huo huku makamu wa rais dkt Philip Mpango akitarajiwa kuwa mgeni rasmi " Alisema


Maadhimisho hayo yatakayohusisha usafi wa Mlima utakaofanyika kwa siku kumi kuanzia machi 1,ambapo wadau wa utalii wapatao 500 watashiriki.


Amesema kuwa Shughuli zingine zitakazofanyika katika sherehe za maadhimisho hayo ni pamoja na ugawaji na upandaji wa miti, zoezi litakalozinduliwa na mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Nurdin Babu.


"Pia tutawatembelea waongoza utalii wa miaka ya 70 ili kuzungumza nao na kupata uzoefu wao na ushauri wao"


Alisema tangu kuanzishwa kwa shughuli za utalii katika mlima Kilimanjaro, mafanikio kadhaa yamepatikana ikiwemo ongezeko la watalii na kufikia elfu 50 kwa mwaka, kuongezeka kwa njia za kupandisha mlima huo kutoka njia moja hadi kufikia njia sita

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top