Na Ferdinand Shayo,Arusha.
Waziri wa Mambo
ya nje wa Ujerumani Heiko Maas ametembelea Ofisi za Umoja wa Mataifa ya
kushughulikia Masuala yaliyoachwa na Mahakama za jinai za umoja wa mataifa
pamoja na kujionea makavati yaliyowekwa kumbukumbu za upelelezi,mashtaka na
mwenendo wa kesi.
Waziri huyo
aliambatana na balozi za Ujerumani
nchini Tanzania alipokuwa katika ziara yake ya siku moja ambapo alipata
kujulishwa juu ya shughuli za za taasisi hiyo ambayo imejikita katika kuwasaka
watuhumiwa ambao bado hawajakamatwa ,kuwalinda waathirika na mashahidi wa
mauaji ya kimbari yaliyotokea nchini Rwanda.
Ziara ya
waziri huyo ni ziara ya kwanza barani Afrika tangu ateuliwe kuwa waziri march 2018 ,ziara
hiyo ni muendelezo wa Nchi ya Ujerumani ambapo amesema kuwa wanafurahi katoa mchango kwa taasisi hiyo ya kimataifa
pamoja na kuimarisha mahusiano kati ya Ujerumani na bara la Afrika.
Afisa Mkuu
wa Mambo ya nje katika taasisi hiyo Ousman
Njikam amemkaribisha Waziri huyo katika jengo la mahakama ambapo shughuli za
kimahakama zinaendeshwa ,mahakama hiyo inaendelea na kazi yake ili kutoa haki
kwa walalamikaji na walalamikiwa .
Msimamizi
Mkuu wa Msajili wa Mahakama Sera Attika amesema kuwa mahakama hiyo ina sehemu
maalumu za maabusu,na maktaba yenye makavati yaliyobeba historia ya Mauaji ya
Rwanda ambayo hutumika kwa utafiti .
Waziri huyo
ametembelea taasisi za kimaitaifa ikiwemo Mahakama ya Haki za binadamu ya
Afrika na Jumuiya ya Afrika Mashariki.
About Author

Advertisement

Related Posts
- FRIEDKIN CONSERVATION FUND WATOA MILLIONI 84 KUSAIDIA MIRADI YA MAENDELEO KWA JAMII YA MOYOWOSI, UVINZA NA UGALA02 Oct 20180
Baadhi ya wakurugenzi na viongozi wa Friedkin Conservation Fund wakiwa katika maonesho ya na...Read more »
- MOBISOL YASHIRIKI SIKU YA USAFI WA MAZINGIRA DUNIANI, WAHIMIZA MATUMIZI YA NISHATI JUA KUTUNZA MAZINGIRA17 Sep 20180
Baadhi ya wafanyakazi wa Mobisol Wakifanya usafi wa mazingira jijini Arusha mapema leo Baadhi ...Read more »
- JERRY MURRO ATOA MKWARA MZITO KWA WANAARUMERU MARA BAADA YA KUAPISHWA31 Jul 20180
Mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo katikati akiwa na wakuu wapya wa wilaya za Arumeru Bwana J...Read more »
- WAANDISHI WAWASILI KWA MGANGA WA JADI ILI KUMUELIMISHA JUU YA MADHARA YA UKEKETAJI KWA WATOTO WA KIKE.01 Jun 20180
Waandishi wa redio jamii tano Tanzania toka katika mikoa minne ya Arusha,Manyara,Dodoma na ...Read more »
- WAMAASAI, WASONJO WATAKIWA KUACHA UKEKETAJI01 Jun 20180
Jamii za Kimaasai na Sonjo zinazopatikana katika wilaya ya Ng...Read more »
- WADAU WA UTALII JIJINI ARUSHA WATOA MSAADA KUBORESHA HUDUMA YA AFYA31 May 20180
WADAU wa utalii mkoani Arusha wamekabidhi msaada wa Vitanda 40 kumi &nbs...Read more »
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.