PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: TAWIRI YAOMBWA KUAINISHA MAENEO YA MAPITO YA WANYAMA KATIKA IKOLOJIA YA TARANGIRE
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
Mhifadhi Mkuu wa hifadhi ya taifa ya Tarangire,Herman Batiho akizungumza na wanahabari juu ya kukabiliwa na changamoto ya kubaki kisiwa...
Mhifadhi Mkuu wa hifadhi ya taifa ya Tarangire,Herman Batiho akizungumza na wanahabari juu ya
kukabiliwa na changamoto ya kubaki kisiwa kutokana na uvamizi wa watu katika baadhi ya maeneo ya hifadhi hiyo
Mhifadhi Mkuu wa hifadhi ya taifa ya Tarangire,Herman Batiho akizungumza na wanahabari juu ya
kukabiliwa na changamoto ya kubaki kisiwa kutokana na uvamizi wa watu katika baadhi ya maeneo ya hifadhi hiyo


Afisa Wanyamapori wa halmashauri ya Babati vijijini, Beatrice Ndanu akizungumza na waandishi wa habari juu ya
uvamizi mkubwa wa shughuli za kibinaadamu,ikiwepo wafugaji,kuanzisha mashamba, majengo na kilimo katika ikolojia ya tarangire na manyara


Afisa mifugo na uvuvi halmashauri ya Babati vijijini Bwana Gilbert Mbesere akizungumza na wanahabari hao

Mhifadhi Mkuu wa hifadhi ya taifa ya Tarangire,Herman Batiho akizungumza na wanahabari juu ya
kukabiliwa na changamoto ya kubaki kisiwa kutokana na uvamizi wa watu katika baadhi ya maeneo ya hifadhi hiyo



Mhifadhi Mkuu wa hifadhi ya taifa ya Tarangire,Herman Batiho akizungumza na wanahabari juu ya
kukabiliwa na changamoto ya kubaki kisiwa kutokana na uvamizi wa watu katika baadhi ya maeneo ya hifadhi hiyo




Mhifadhi Mkuu wa hifadhi ya taifa ya Tarangire,Herman Batiho akiagana na wanahabari Andrea Ngobole mmiliki wa blog ya princemedia, Mussa Juma wa gazeti la mwananchi na Janeth Mushi wa gazeti la Mtanzania na wengineo waliomtembelea ofisini kwake mapema wiki hii kujua changamoto za shughuli za kibinadamu wanaozunguka hifadhi hiyo

 


Mkurugeni wa chemchem foundation Ricardo Toss akizungumza na wanahabari hao juu ya changamoto zinazotokana na shughuli za jamii katika maeneo hayo
Charles sylvester meneja wa chemchem  foundation akizungumza na wanahabari hao
NA: ANDREA NGOBOLE, PMT

Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori(TAWIRI),imeombwa kusaidia kuanisha maeneo ya mapito ya wanyama katika eneo la Ikolojia ya Tarangire na Manyara, ili kuzuia uharibifu na uvamizi wa maeneo hayo ambao unaendelea.

Eneo la ikolojia ya Tarangire na Manyara lina ukubwa kwa kilomita za mraba 35,000 ambapo sasa eneo kubwa la nje ya hifadhi limevamiwa na shughuli za kibinaadamu,ikiwepo kilimo, ufugaji na makazi.

Afisa Wanyamapori wa halmashauri ya Babati vijijini, Beatrice Ndanu, akizungumza na waandishi wa habari, alisema baada ya wizara ya Maliasili na Utalii, kutoa kanuni za ulinzi wa mapito ya wanyamapori, sasa wanasubiri TAWIRI kuanisha mapito hayo ili yasimamiwe.

Ndanu alisema, katika eneo la ikolojia ya Tarangire na Manyara, kuna uvamizi mkubwa wa shughuli za kibinaadamu,ikiwepo wafugaji,kuanzisha mashamba, majengo na kilimo.

Mkurugenzi wa taasisi ya  uhifadhi ya Chemchem foundation, Riccardo Tossi, ambao wamewekeza katika eneo la hifadhi ya jamii ya Burunge lilipo kati kati yaTarangire na Manyara, alisema wapo tayari kushirikiana na serikali kuwezesha kuanishwa maeneo ya mapito ya nyama.

"tunapata shida katika uwekezaji, kuna mifugo na makazi ndani ya hifadhi hivyo imekuwa ni changamoto katika kupambana na ujangili"alisema

Mhifadhi Mkuu wa hifadhi ya taifa ya Tarangire,Herman Batiho alisema hifadhi hiyo ambayo iliyoanzishwa mwaka 1970, ikiwa na ukubwa wa kilomita za mraba 2850 inakabiliwa na changamoto ya kubaki kisiwa kutokana na uvamizi wa watu.

Alisema watu wamevamia maeneo ya mapito ya wanyama na kufanya shughuli za kibinadamu ambazo zina athari kwa wanyamapori na kuendelea kuwepo hifadi hizo.

"tunaomba mapito ya wanyama kuanishwa na kulindwa lakini pia kudhibiwa watu ambao wamekuwa wakiharibu vyanzo vya maji na kufanya shughuli ikiwepo kilimo na ufugaji katika maeneo ya hifadhi"alisema

Mwenyekiti wa jumuiya ya hifadhi ya jamii ya wanyamapori(WMA) ya BURUNGE, Ismail Ramadhani, alisema ongezeko la watu na mifugo,imekuwa ni tatizo katika uhifadhi hasa kutokana na kuongezeka uvamizi katika maeneo yaliyohifadhiwa.

Hata hivyo, alisema hivi sasa kuna mkakati wa vijiji vyote ambavyo vipo katika eneo la Burunge  WMA, kupimwa na kuanzisha mpango wa matumizi bora ya ardhi, ambayo itawezesha kutengwa maeneo ya hifadhi na shughuli za kijamii.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top