PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: Serikali yafuta leseni zote za kuhodhi maeneo ya madini na kuwataka wamiliki kuomba upya wakizingatia Sheria na Kanuni mpya za Madini
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
Serikali imefuta leseni zote za kuhodhi maeneo ya madini na wamiliki wake wametakiwa kuomba upya wakizingatia Sheria ya Madi...


Serikali imefuta leseni zote za kuhodhi maeneo ya madini na wamiliki wake wametakiwa kuomba upya wakizingatia Sheria ya Madini na kanuni zake.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Ijumaa Mei 11, 2018 Mwenyekiti wa Tume ya Madini nchini, Profesa Idris Kikula amesema tangazo la Serikali namba moja la mwaka 2018 limesema maeneo yote yaliyopewa leseni yanarejeshwa serikalini bila hakikisho la kupewa tena.

Amesema uamuzi huo umefanyika kwa mujibu wa Sheria ya Madini ya mwaka 2010 ikisomwa na marekebisho yake ya mwaka 2017 na kanuni ya 21 ya kanuni za Madini (Haki Madini za mwaka huu).

Amesema leseni zilizofutwa na wamiliki wake wanatakiwa kuomba tena zinazihusu kampuni 11, kwamba leseni hizo zinajumuisha migodi ya kati na mikubwa.

Migodi hiyo ni pamoja na Kabanga Nickel Company Limited, National Mineral Development Corporation Limited, Bafex Tanzania Limited ambayo inamiliki leseni za maeneo matatu.

Nyingine ni Mabangu Mining Limited, Resolute (Tanzania) Limited, Wigu Hill Mining Company Limited, Nachingwea Nickel Limited na Precious Metals Refinery Company Limited.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top