PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: RC GAMBO KUWA MGENI RASMI KATIKA TAMASHA LA WANAHABARI MKOANI ARUSHA JUMAPILI HII
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
Katibu wa Taswa Arusha Mussa Juma aliyesimama akitangaza tamasha la wanahabari mkoani Arusha juu ya bonanza la kumi na mbili litakalof...


Katibu wa Taswa Arusha Mussa Juma aliyesimama akitangaza tamasha la wanahabari mkoani Arusha juu ya bonanza la kumi na mbili litakalofanyika jumapili hii ya october 15, 2017 katika viwanja vya general Tyre jijini Arusha, wengine ni mwenyekiti wa Taswa Arusha Jamila Omary  wa pili kutoka kushoto na wa pili kutoka kulia ni afisa malalamiko wa mfuko wa hifadhi ya jamii LAPF mkoani Arusha Bwana Mwaijibe ambao ni wadhamini wa tamasha hilo.


Godfrey Amani kulia ambaye ni Afisa mauzo wa kampuni ya vinywaji baridi vya jamii ya cocacola Bonite Bottlers LTD, mkoani Arusha akimkabidhi vinywaji katibu wa Taswa mkoani Arusha Mussa Juma kama sehemu ya udhamini wao  kwa ajili ya bonanza la wanahabari litakalofanyika jumapli hii ya october 15, 2017 katika viwanja vya General Tyre jijini Arusha.


Meneja wa LAPF kanda ya kaskazini RAJABU KINANDE kulia  akimkabidhi Tshirt katibu wa taswa mkoani Arusha Mussa Juma kwa ajili ya Tamasha la 12 la wanahabari mkoani Arusha litakalofanyika October 15, 2017 katika viwanja vya General Tyre jijini Arusha.


 
 NA: ANDREA NGOBOLE, PMT

Arusha, Tamasha la waandishi wa habari, kanda ya kaskazini, linatarajiwa kufanyika jumapili, octobar 15 katika uwanja wa General Tyre ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Mkuu wa mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo.

Katika tamasha hilo, ambalo litashirikisha wanahabari zaidi ya 500, kutoka mikoa ya Arusha, Tanga, Manyara na Kilimanjaro,limedhaminiwa na shirika la hifadhi za Taifa(TANAPA) Mifuko ya hifadhi ya Jamii ya LAPF na PSPF, Mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro, kampuni ya vinywaji baridi ya Coca cola na kampuni ya ya vinywaji baridi ya SBC (T) Limited na Palace Hoteli.

Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari, Katibu wa TASWA mkoa wa Arusha, Mussa Juma, alisema tamasha hilo, limeandaliwa na TASWA kwa kushirikiana na kampuni ya Arusha media na maandalizi yote yamekamilika.

Juma alisema katika tamasha hilo, bingwa atazawadiwa kikombe na fedha taslimu jumla ya shilingi 500,000, mshindi wa pili fedha taslimu 100,000 na kwa upande wea mpira wa pete mshindi ni kikombe na fedha taslimu jumlaya sh 300,000 na mshindi wa pili sh 50,000.

Alisema pia kutakuwa na michezo ya mbio za magunia, kuvuta kamba, mbio za vijiko, riadha na masumbwi ambapo tayari waambuzi wanaotambuliwa na mashirika mbali mbali ya michezo watakuwepo.

Hata hivyo, alisema wadhamini wengine wa tamasha hilo wanatarajiwa kutangazwa, ili kuhakikisha wanahabari wanaburudika ambapo pia kuwa kuwa na benki maalum ambayo itatumnbuiza siku za tamasha.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa TASWA Arusha, Jamila Omar alitoa wito kwa wanahabari wote na familia zao kujitokeza katika tamasha hili ambalo hufanyika kila mwaka mkoani Arusha.

Alisema kauli mbiu ya tamasha hilo, ambalo linaendama na maadhimisho ya kumbukumbu ya mwalimu nyerere ni michezo ni ajira, michezo ni kazi tufanye kazi kwa bidii kuunga mkono jitihada za serikali ya awamu ya tano ya Tanzania ya viwanda.

Mratibu wa Tamasha hilo, Andrea Ngobole alizitaja timu ambazo zitashiriki kuwa ni TASWA Dar es Salaam, Triple A,RadioSunrise , chuo cha uandishi habari cha Arusha(AJTC)timu ya Arusha One Fm, TASWA Arusha,Radio ORS ya Manyara ,NSSF na timu ya Wazee Klabu.


About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top