PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: MFAHAMU Rais Mpya wa Ufaransa Emmanuel Marcon..Amemuoa Mwalimu Wake Aliyemzidi Zaidi ya Miaka 24..Alianza Kutembea Naye Toka Akiwa na Miaka 17..!!
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
EMMANUEL MARCON mwenye umri wa miaka 39 ndiye anayetarajiwa kuwa rais ajaye wa Ufaransa. Pamoja na hayo, Marcon ambaye ameoa mke mw...

EMMANUEL MARCON mwenye umri wa miaka 39 ndiye anayetarajiwa kuwa rais ajaye wa Ufaransa.

Pamoja na hayo, Marcon ambaye ameoa mke mwenye umri wa miaka 64 ,ana mambo mengi ya kufurahisha na kuvutia maishani mwake hususan kuhusiana na mkewe huyo ambaye anamzidi umri kwa kiasi cha miaka  zaidi ya 24.

Mkewe huyo alikuwa ni mwalimu wake wa darasa miaka ipatayo 24 iliyopita ambapo mwalimu wake wa darasa wakati huo alikuwa na binti ambaye alikuwa mwanafunzi mwenzake darasa moja.  Wakati huo, kila mtu, wakiwemo wazazi wake Marcon, walifikiri binti huyo wa mwalimu alikuwa rafiki yake, wakati hawakuwa hivyo.

Katika mlolongo huo wa vituko, Marcon alijikuta katika mapenzi na mwalimu wake wakati yeye akiwa na umri wa miaka 15 ambapo wakati huo, mwalimu huyo alikuwa ameolewa akiishi kwa furaha na akiwa na watoto watatu

Alipofikisha umri wa miaka 17, aliamua kumuoa mwalimu huyo, wakati huo akiwa na umri wa miaka 42.

apendanao hao walifunga pingu za upendo mwaka 2007 wakati huo ‘mlume’ huyo akiwa na umri wa miaka 30 na ‘mrembo’ wake akiwa anapiga hodi katika umri wa miaka 55.

Mwanandoa huyo wa kiume anatarajiwa kuapishwa kuwa Rais wa Ufaransa mwezi ujao akiwa amebakiza miezi sita kufikisha umri wa miaka 40 wakati ambapo kipenzi chake, yaani mkewe,  ana watoto  (watu wazima) watatu na wajukuu saba sasa.

Ni vyema pia kufahamu kwamba mtoto wa kwanza wa mkewe huyo anamzidi Marcon kwa umri wa miaka miwili, wakati ambapo mtoto wake wa pili, aliyekuwa kipenzi na mwanafunzi mwenzake  na Marcon wakiwa darasa moja, wanalingana umri.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top