PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: KUPENDA MAFANIKO NA KUTAFUTA MAFANIKIO NI VITU VIWILI TOFAUTI....
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
NA: ANDREA A. NGOBOLE PMT Kila binadamu mwenye akili timamu hupenda kufanikiwa ili kuwa na maisha mazuri yenye kupata hitaji lake ...


Image may contain: 1 person, suit
NA: ANDREA A. NGOBOLE PMT
Kila binadamu mwenye akili timamu hupenda kufanikiwa ili kuwa na maisha mazuri yenye kupata hitaji lake la moyo na  yampendezayo kila mara  ila ni binadamu wachache sana wanaotafuta mafanikio ya kweli na kufanikiwa kimaisha na hapo ndio linapotokea gape kubwa kati ya walio nacho na wasiokuwa nacho nina maana hapo ndiyo tofauti iliyopo kati ya maskini na tajiri.

Mtu asiyetafuta mafanikio ni mtu mwenye sifa zifuatzo kwanza ni mvivu wa fikra hapendi kuishughulisha akili yake katika kutafuta mafanikio huishia kuwa na malalamiko na kuona changamoto ndani ya jamii yake badala ya kuona fursa katika changamoto inayoikabli jamii, hupenda kujadili watu na maisha yao badala ya kujadili namna gani ya kuweza kufanikiwa kiuchumi, hupenda kutumia Zaidi ya akipatacho katika pesa zake, hupenda kukopa na kushindwa kulipa deni na hivyo kujiongezea maadui badala ya marafiki, huona aibu kufanya kazi anayodhani inamzalilisha na mwisho wa siku huishia kuugulia maumivu ya jeraha la moyo kwa kukosa pesa na kutafuta visingizio visivyo na kichwa wala miguu mfano serikali imebana pesa au ajira ngumu kupata wakati anamiliki simu ya gharama kubwa.

Watu wasiofikiria mafanikio hufikiria Zaidi katika njia za mkato na kudhani njia hizo za mkato zitamletea mafanikio maishani, mfano mwanafunzi asiyejiandaa na masomo yake vizuri ategemee aje anunue mtihani afaulu masomo yake huenda akafanikiwa ila ni kwa muda mfupi sana kwani uwezo utakuwa mdogo katika utendaji wake wa kazi.

Mfano mfanyabiashara asiyelipia kodi biashara yake kwa kutaka short cut ya kufanikiwa siku akigundulika huenda biashara yake ikafa kabisa kwani atafilisiwa na mamlaka husika za utozaji wa kodi na ndio hao ambao hufikiria Zaidi kuhonga ili kupitisha mzigo siku njia zikibanwa ndio hao utasikia anafunga biashara na kutoa visingizio kwa serikali iliyopo madarakani.
Asiyefikiria mafanikio vema hawezi kufuata utaratibu uliowekwa  wa kutenda kazi zake vizuri bali huishia kufanya kwa mazoea na hivyo kuonekana hana umuhimu wowote na ndio huwa wa kwanza kufikiria kutumbuliwa na wenye mamlaka ya kumtumbua.

Ni sawa na mtu ambaye wiki nzima hajafanya kazi yoyote ya kumuingizia kipato lakini huyo huyo anafikiria weekend kutoka  na kwenda kula starehe katika kumbi za starehe na burudani za muziki wa dansi au wa kizazi kipya ina maana anapenda starehe lakini hapendi kufanya kazi huyu mafanikio atayasikia kwenye  bomba tu hawezi kufanikiwa kwani mafanikio hayampendi mtu asiyeyatafuta.  

Mtu anayetafuta mafanikio ana muda mchache sana wa kulala kwani yeye hufikiria Zaidi ni jinsi gani atajikwamua kiuchumi kwa kubuni miradi midogomidogo itakayomuingizia kipato cha uhakika, hujadiliana mambo ya msingi ya kufanya ili aweze kujiongezea kipato chake halali, hawaamini katika njia ya mkato ili kufanikiwa, hujituma kila siku za maisha yao kuhakikisha wanapata kile kinachwaongezea kipato chao cha kila siku.

Mfano kilimo hakihitaji njia ya mkato lazima uandae shamba, ulime kwa trekta au plau, upande mbegu uweke mbolea na umawagilie maji mbegu ili ziote na zikishaota lazima upalilie na usubiri kwa muda flani ndio upate mazao husika na kuvuna mazao yako na mafanikio pia yanahitaji uvumilivu huo kama wa mkulima mwenye busara ya kujituma ipasavyo na kuamini atapata mazao ya kile alichopanda.

Ili ufanikiwe inakulazimu kwanza kujitengenezea jina la biashara yako mwenyewe yaani wewe mwenyewe uwe biashara kama una kipaji cha kuimba imba sana itengeneze sauti yako iwe bora nay a kuvutia, kama ni kucheza mpira cheza sana na ufanye mazoezi mpaka uwe tegemeo kwa timu yako na wengine wakuone pia, kama kudansi fanya mazoezi ya kutosha kukuza kipaji chako ili kikulipe kwani kila mmoja wetu ana kipawa chake chenye uwezo tofauti na mwezake ndiyo maana tuna wanamuziki wengi lakini wenye vipaji vyao wamedumu mpaka leo tunasikiliza nyimbo zao kama wakina Marijani Rajabu na wachezaji mpira bora kabisa kama Pele na wengineo.

Mtu anayetafuta mafanikio huwekeza katika kutafuta maarifa kila siku yatakayomfanikisha kujua namna ya kujikwamua kiuchumi yaani husoma sana vitabu vyenye maarifa ya ujasiriamali, haogopi kuuliza maswali ya msingi yatakayompa majibu sahihi kwa biashara ama kazi yake toka kwa watu anaoamini kuwa wana maarifa sahihi, huambatana na watu wanaofanana kifikra ili kujiongezea fikra chanya za mafanikio yake na hupenda sana kujiridhisha kabala ya kuwekeza katika biasharea flani pia wote wanazungumza lugha moja ya biashara wanamaneno yenye mvuto masikioni mwa wateja hawaongei lugha za mtaani.

Huwatambua wateja wake na hata wakiongezeka huwa hawaridhiki nao hutafuta wateja wapya kila siku na hujitathmini kila siku juu ya biashara yake na yeye mwenyewe kama yupo katika njia sahihi na kama amekosea wapi ili ajirekebishe kukidhi matakwa ya biashara yake na mafanikio yake.
Ni laz\ima tuamue sasa kubadilika kwa kutafuta mafanikio na sio kupenda mafanikio ukiyapenda bika kuwekeza katika kuyatafuta huenda ukaishia kuwa mtu wakawaidza kama walivyo wengine ni lazima sasa uwe mbuni miongoni mwa ndege ili utambulike na wanakuona.

Kuwa na wakati mwema na Mungu akubariki sana kwa kukubali kupitia hapa princemedia tz

ASANTE KWA KUSOMA MAKALA HII UKIWA NA SWALI, MAONI AU USHAURI USISITE KUWASILIANA NAMI
NGOBOLE, Andrea Ashery.
0755780131
facebook.com/ Andrea Ngobole
facebook page, instergram na twiter ni  princemediatz



About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top