![]() |
Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wakiwa kwenye mkutano huo. |
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dk. Mpoki Ulisubisya (kushoto), akihutubia wakati akizindua Baraza la tatu la Wafanyakazi wa Bohari ya Dawa (MSD), Dar es Salaam leo.
Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi MSD, ambaye ni Mkurugenzi Mkuu wa MSD Laurean Bwanakunu (kulia), akizungumza kwenye mkutano huo.
Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wakifuatilia kwa makini yaliyokuwa yakielezwa na viongozi wao katika mkutano huo.
Na Dotto Mwaibale
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dk. Mpoki Ulisubisya amewaasa watumishi wa Bohari ya Dawa (MSD) kuhakikisha kuwa wanatekeleza majukumu yao ipasavyo ili kupunguza malalamiko ya wananchi juu ya ukosefu wa dawa.
Katibu Mkuu huyo ameyasema hayo Dar es Salaam leo wakati akizindua Baraza la tatu la Wafanyakazi la Bohari ya Dawa (MSD) ambapo pia amesisitiza kuwa Baraza hilo libuni mbinu na mikakati mbadala za kuboresha utendaji bila kusahau kutii miiko ya utumishi wa umma.
Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi MSD, ambaye ni Mkurugenzi Mkuu wa MSD Laurean Bwanakunu amemweleza Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya kuwa tayari MSD imeanza kununua dawa na vifaa tiba kutoka kwa wazalishaji, ambapo hadi sasa wanawazalishaji 20 ambao wanamikataba, na wazabuni wengine 76 wadawana 79 wa vifaa tiba zabuni zao zinaandaliwa.
Mkutano huo umehudhuriwa na wajumbe kutoka Makao Makuu ya MSD na Kanda zote nane za MSD ambao ni pamoja na Mwenyeviti wa Tughe na matawi pamoja wawakilishi wa wafanyakazi.
About Author

Advertisement

Related Posts
- WADAU WA UTALII JIJINI ARUSHA WATOA MSAADA KUBORESHA HUDUMA YA AFYA31 May 20180
WADAU wa utalii mkoani Arusha wamekabidhi msaada wa Vitanda 40 kumi &nbs...Read more »
- WAZIRI UMMY MWALIMU: RMO,DMO TENGENI SIKU ZA UCHUNGUZI WA SARATANI29 Apr 20180
WAZIRI wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Ummy Mwalimu akizungumza leo Jijini Tan...Read more »
- Rekodi ya Madaktari Wanaomtibu Tundu Lissu Ubelgiji Usipime Kabisa, wanategemewa na bara zima la ulaya20 Mar 20180
Rekodi ya Madaktari Wanaomtibu Tundu Lissu Ubelgiji Usipime Kabisa HUU ndio...Read more »
- WAZIRI WA AFYA AKIRI CHANGAMOTO YA UHABA WA MADAKTARI17 Jan 20180
Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii WAZIRI wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jin...Read more »
- TABIA ZA KUEPUKA ILI UWE MWENYE AFYA BORA19 Dec 20170
Na Jumia Food Tanzania Chakula huupatia mwili virutubisho ili uweze kufanya kazi kwa ufasah...Read more »
- PITIA HAPA UFAHAMU FAIDA MBALIMBALI ZA TANGAWIZI KATIKA MWILI WA BINADAMU04 Dec 20170
Hicho ni kiungo kinachotokana na mzizi wa mmea unaoitwa Tangawizi. Ni mmea unaofanana sa...Read more »
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.