PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: Degree/Diploma sio Kazi Sehemu ya nne
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
NA ADSON KAGIYE Fursa nyingi huja na kutoweka, zingine hudumu kwa kitambo, zingine hudumu kwa karne. Mfano soda ya cocacola i...
https://lh6.googleusercontent.com/-xIpjgqv2UcA/AAAAAAAAAAI/AAAAAAAAAAA/F_1A0MyWG1s/s128-c-k/photo.jpg
NA ADSON KAGIYE


Fursa nyingi huja na kutoweka, zingine hudumu kwa kitambo, zingine hudumu kwa karne. Mfano soda ya cocacola imekuwa Sokoni tangu mwanzo mwa karne hii.
Fursa huenda na utayari wa MTU, ni kama mbegu, ukipanda kwenye mwamba wenye Maji itaota lakini haitakuwa na kuzaaa, ukipanda kwenye pori itaota na kukua na kutoa mazao hafifu na ukipanda kwenye udongo mzuri inaota na kuzaa.
Na ndio mana utasikia ukifa maskini ni kosa lako mwenyewe kwa kuwa ulikuwa hujajiandaa kuipokea fursa, hukuandaa mazingira mazuri ya kuipokea fursa, hukuwa tayari kuitunza fursa na wakati wa mavuno ulipokaribia uliwaachia ndege wale mavuno yako
HATARI KUBWA SI KUTOKUONA FURSA Bali ni kutokujiandaa kuiona fursa. Yaani unakuta mtu anaziba masikio yake hataki hata kuelezwa fursa yeyote.
Kama cocacola wasingeweza kuona fursa ktk soko la vinywaji, wakspambani kutengeneza brand yao na kuwa mstari wa mbele ktk jamii basi Leo hii usingeisikia cocacola Tanzania.
JE UKIPEWA FURSA UTAIFANYIA KAZI, AU UTABAKIA KUSEMA NIPO BIZE?
Na Adson Kagiye

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top