Na Ferdinand Shayo,Arusha.
Taasisi
isiyo ya kiserikali ya Wanaume Kazini
maarufu kama Man at Work imelaani vikali vitendo vya ushoga vinavyoshusha hadhi
na thamani ya wanaume hivyo wameitaka serikali kupiga vite vitendo hivyo
ambavyo ni kunyume cha Maadili ya Tanzania na Afrika kwa Ujumla.
Muasisi wa
Taasisi hiyo yenye makao yake jijini
Arusha Maxwell Stanslaus amesema kuwa Wanaume kazini wanapinga vikali
vitendo vya ushoga kwa zaidi ya Asilimia 100% na kuwataka wanaojihusisha na
vitendo hivyo kuacha Mara moja.
Maxwell
alisema hayo jana katika mkutano Mkuu wa Wanaume kazini uliofanyika jijini hapa
huku akisema kuwa taasisi hiyo imelenga kuhimiza wanaume kote nchini kutimiza
wajibu wao na kutenda majukumu yao kama wanaume katinga ngazi ya familia,jamii
na taifa ili kuchochea maendeleo.
“Kwa sasa
tunaona nidhamu ya serikali imerudi kutokana na Mwanaume mmoja tu Rais John
Pombe Magufuli kuamua kutimiza wajibu yake hivyo Basi Wanaume zaidi ya Milioni walioko Tanzania wakiamua kutimiza majukumu
yao na wajibu Tanzania itanyooka” Alisema Maxwell
Moja kati ya
Wanaume waliohudhuria ni Joseph Mayagila alisema kuwa matatizo ya ushoga
yanatokana na baadhi ya wanaume kujisahau na kujaribu kuwa wanawake ,jukwaa
hili la wanaume ni muhimu kuwakumbusha wanaume juu ya uanaume wao na kutimiza
yale yanayowapasa kama wanaume.
Dokta
Emmanuel Buganga ameeleza kuwa vuguvugu
la wanawake kudai haki zao linatokana na baadhi ya wanaume kutotimiza wajibu
wao kama wanaume wameacha majukumu yao ya kutunza familia zao na kuwa walezi na
walinzi wa familia .
Mhamasishaji
wa Masuala ya kijamii Samuel Sasali amesema kuwa wanaume wengi wamejisahau sana
katika masuala ya malezi ya familia kwani usimpolea mtoto katika njia impasayo
atakuja kukuaibisha ukubwani.
About Author

Advertisement

Related Posts
- FRIEDKIN CONSERVATION FUND WATOA MILLIONI 84 KUSAIDIA MIRADI YA MAENDELEO KWA JAMII YA MOYOWOSI, UVINZA NA UGALA02 Oct 20180
Baadhi ya wakurugenzi na viongozi wa Friedkin Conservation Fund wakiwa katika maonesho ya na...Read more »
- MOBISOL YASHIRIKI SIKU YA USAFI WA MAZINGIRA DUNIANI, WAHIMIZA MATUMIZI YA NISHATI JUA KUTUNZA MAZINGIRA17 Sep 20180
Baadhi ya wafanyakazi wa Mobisol Wakifanya usafi wa mazingira jijini Arusha mapema leo Baadhi ...Read more »
- JERRY MURRO ATOA MKWARA MZITO KWA WANAARUMERU MARA BAADA YA KUAPISHWA31 Jul 20180
Mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo katikati akiwa na wakuu wapya wa wilaya za Arumeru Bwana J...Read more »
- WAANDISHI WAWASILI KWA MGANGA WA JADI ILI KUMUELIMISHA JUU YA MADHARA YA UKEKETAJI KWA WATOTO WA KIKE.01 Jun 20180
Waandishi wa redio jamii tano Tanzania toka katika mikoa minne ya Arusha,Manyara,Dodoma na ...Read more »
- WAMAASAI, WASONJO WATAKIWA KUACHA UKEKETAJI01 Jun 20180
Jamii za Kimaasai na Sonjo zinazopatikana katika wilaya ya Ng...Read more »
- WADAU WA UTALII JIJINI ARUSHA WATOA MSAADA KUBORESHA HUDUMA YA AFYA31 May 20180
WADAU wa utalii mkoani Arusha wamekabidhi msaada wa Vitanda 40 kumi &nbs...Read more »
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.