PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: Mashabiki Wakerwa na Kauli Hii ya Zari, Wadai Amewakejeli Maskini
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
Labda ukweli unauma.. Kwamba wengi tunatamani sana maisha mazuri anayoishi D...

Labda ukweli unauma.. Kwamba wengi tunatamani sana maisha mazuri anayoishi Diamond na mchumba wake, Zari the Bosslady. Wapo wanaoishia kutamani na kumuomba Mungu nao waje kuwa na maisha hayo, wengine hushukuru na hufurahi tu kwa kile walichonacho ama tumeseme wameridhika na kidogo wanachopata.

Lakini wapo ambao hushindwa kujizuia kupata wivu na kuwachukia tu watu wenye mafanikio – wa kuitwa haters. Hayo ni majaribu makubwa waliyonayo mastaa duniani. Lakini sio mara zote huvumilia matusi na kejeli wanazozipata kwenye mitandao ya kijamii.

Wakati Zari akiendelea kula raha Ulaya na mchumba wake Diamond, ameendelea kutupiwa vijembe na watu kuwa hawajali tena wanae watatu aliowaacha Afrika Kusini, kwamba kila siku kiguu na njia na Diamond. Hilo limemkera, na ameamua kulijibu.

Staa huyo amepost picha hiyo juu na tafsiri yake kwa maneno hayo ni:

Watoto wangu wameniuliza, kwanini kila mtu amechukia? Nimewaambia tuna vitu ambavyo hawana. Wakati mnachukua, mimi naenda mall, kumwaga fedha. Naweza, huwezi

Lakini pia aliweka caption isemayo: Baadhi yenu hamtaelewa hili lakini ni sawa. Ninawajibika kwa ninachoandika, na sio unavyokielewa.


Hilo limeonakana kuwakera wengi, wakiwemo mashabiki wake. Baadhi waliongea mambo mazito kiasi cha kumfanya awajibu pia.


Well, good news ni kubwa ex wake, Ivan, amewachukua wanae na kuwapeleka kwenye kisiwa cha maraha cha Ibiza kula pizaa! So waswahili wanasema hiyo ni ngoma drooo… Pesa inaongea!!

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top