PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: Maalim Seif Aiondoa Familia yake Zanzibar na Kuipeleka Muscat Oman
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
Pichani ni mkewe Seif Shariff Hamad, Bi Awena Sinani Masoud akiwa chumba cha VIP uwanja wa ndege na tiketi yake ya Oman ...


Pichani ni mkewe Seif Shariff Hamad, Bi Awena Sinani Masoud akiwa chumba cha VIP uwanja wa ndege na tiketi yake ya Oman Air, muda mfupi kabla ya kuondoka.

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar na Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Seif Shariff Hamad ameondosha familia yake katika Kisiwa cha Unguja na kuipeleka Muscat-Oman.

Familia hiyo ya Maalim Seif Shariff Hamad wameondoka juzi jioni kwa kutumia ndege ya Shirika la ndege la Oman (Omar Air). Familia hiyo ya Maalim Seif wameondoka katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere International Airport saa 11:50 jioni juzi.

Haikuweza kufahamika mara moja sababu hasa za Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Seif Shariff Hamad kuiondoa familia yake Zanzibar. Kwa sasa Makamu huyo wa Kwanza wa Rais yupo katika mapumziko katika Hoteli ya Kitalii ya Dar es Salaam Serena.

Chanzo: ZanzibarNews.net

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top