PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: Flaviana Matata Amjia Juu Anayedai Kumfikisha Alipo Kwenye Mafanikio yake
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
​ Nimesoma nukuu inayosema kwamba binadamu siku zote tunapenda kupata sifa isiyo stahili kwa mazuri tu lakini...


Nimesoma nukuu inayosema kwamba binadamu siku zote tunapenda kupata sifa isiyo stahili kwa mazuri tu lakini mabaya tunasingizia bahati mbaya. ​
We always take credit for the good and attribute the bad to fortune. Maneno haya yamenichoma moyoni kwani nimeona kuwa yana ukweli katika maisha yetu ya kila siku. Nimefanya kazi siku zote bila kujali mwenzangu au wenzangu wanafanya nini, na sipendi kutangaza mafanikio yangu yote. ​
Ila kuna watu maishani ambao wamenisaidia kufika hapanilipo na hata wao huwa wanaishi kwa kufuata msingi wa kuwa “tendawema uende zako”, na hawajawahi kukaa na kujitangazia kuwa wao ndo wamenifikisha hapa nilipo ingawa ni kweli. ​
Cha ajabu ni pale kuona kuwa kuna mtu ambaye namfahamu kawaida tu na hatuna mazoea wala hajuiniishivyona nimefika vipi hapa nlipo inasemekaana kuwa yeye ndo kanifikisha hapa nilipo. Kibaya zaidi si kuwa kaongea hadharani na marafiki zake bali ni kuiweka bayana katika gazeti. ​
Kitendo hiki kimenishtua na kunisikitisha kwanimimi binfasi sijawahi kuongea katika magazeti kuhusu maisha ya mtuwala kudai kuwa mi ndo nimemfikisha mahala fulani. Lakini chakusikitisha zaidi, watu ambao kweli wamenisaidia katika maisha yanguhawajawahi kukaa na ‘kuuza sura’ kwa kutumia jina langu. ​
Mafanikio yangu madogo nilonayo sasa ndani na nje ya nchi yamefikiwa kwa juhudi zangu na zawatu wachache, hii ni pamoja na kupatikana kwa mkataba wangu wa nje(Afrika Kusini) na mkataba na maelewano yote ni kati yangu mimi,kampuni yangu ya Afrika Kusini na kampuni yangu mama ya CompassCommunications. ​
Hatua zozote zilizochukuliwa hazikumhusisha mtanzaniamwingine. Na hata katika siku zijazo, itaendelea kuwa hivyo. Kwaheshima na taadhima naomba mhusika na wahusika, waache kuongeleamaisha yangu, mafanikio yangu, kwani haiwahusu. ​
Pia naomba wanajamii wenzangu mkisikia kitu kinazungumzwa ambacho hakijatoka kwangu au kampuni yangu mama, basi wajue atakuwa ni binadamu mwingine ambaye ametetereka na kuingia katika mtego ule wakutaka kupata sifa asizostahili.​
Mwisho kabisa napenda kuwashukuru wote ambao wapo sambamba na watanzania wote kwa ujumla ​
Regards,​
Flaviana Matata​

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top