Title: NMB na Kampuni ya John Deere Kutoa Mikopo Rahisi kwa Wakulima
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5
Des:
...
Mkuu
wa Kitengo cha Wateja Wakubwa wa Benki ya NMB, Filbert Mponzi
(kushoto), Mkurugenzi Mtendaji wa Lonagro Tatnzania Ltd, Lukas Botha
(katikati) na Mkurugenzi wa Kampuni ya John Deere, nchi za Afrika Kusini
mwa Jangwa la Sahara, Antois van der Westhuizen (kulia) wakipiga picha
ya kumbukumbu mara baada ya kusaini hati ya makubaliano na Benki ya NMB
itakayo wawezesha wakulima kupata mkopo wa matrekta kwa ajili ya
shughuli zao.Kutoka
kulia ni Mkuu wa Kitengo cha Wateja Wakubwa wa Benki ya NMB, Filbert
Mponzi, Mkurugenzi Mtendaji wa Lonagro Tatnzania Ltd, Lukas Botha na
Mkurugenzi wa Kampuni ya John Deere, nchi za Afrika Kusini mwa Jangwa la
Sahara, Antois van der Westhuizen wakiwa katika tukio hilo lilifanyika
jana kwenye Hoteli ya Golden Tulip jijini Dar es Salaam.Sehemu
ya waandishi wa habari wakishuhudia hafla ya kutiliana saini ya
makubaliano kati ya Benki ya NMB na Kampuni ya John Deere (wauzaji wa
matrekta) kuwawezesha wakulima kupata mkopo wa matrekta kwa ajili ya
shughuli zao. Tukio hilo lilifanyika jana kwenye Hoteli ya Golden Tulip
jijini Dar es Salaam.Sehemu
ya wanufaika wa mkopo huo wakishuhudia hafla ya kutiliana saini ya
makubaliano kati ya Benki ya NMB na Kampuni ya John Deere (wauzaji wa
matrekta) kuwawezesha wakulima kupata mkopo wa matrekta kwa ajili ya
shughuli zao. Tukio hilo lilifanyika jana kwenye Hoteli ya Golden Tulip
jijini Dar es Salaam.Mkurugenzi
Mtendaji wa Lonagro Tatnzania Ltd, Lukas Botha akizungumza katika tukio
la kutiliana saini ya makubaliano kati ya Benki ya NMB na Kampuni ya
John Deere (wauzaji wa matrekta) kuwawezesha wakulima kupata mkopo wa
matrekta kwa ajili ya shughuli zao. Tukio hilo lilifanyika jana kwenye
Hoteli ya Golden Tulip jijini Dar es Salaam.Mkuu
wa Kitengo cha Wateja Wakubwa wa Benki ya NMB, Filbert Mponzi
akizungumza katika tukio la kutiliana saini ya makubaliano kati ya Benki
ya NMB na Kampuni ya John Deere (wauzaji wa matrekta) kuwawezesha
wakulima kupata mkopo wa matrekta kwa ajili ya shughuli zao. Tukio hilo
lilifanyika jana kwenye Hoteli ya Golden Tulip jijini Dar es Salaam.Mkurugenzi
wa Kampuni ya John Deere, nchi za Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara,
Antois van der Westhuizen akizungumza katika tukio la kutiliana saini ya
makubaliano kati ya Benki ya NMB na Kampuni ya John Deere (wauzaji wa
matrekta) kuwawezesha wakulima kupata mkopo wa matrekta kwa ajili ya
shughuli zao. Tukio hilo lilifanyika jana kwenye Hoteli ya Golden Tulip
jijini Dar es Salaam.
Sehemu
ya waandishi wa habari wakishuhudia hafla ya kutiliana saini ya
makubaliano kati ya Benki ya NMB na Kampuni ya John Deere (wauzaji wa
matrekta) kuwawezesha wakulima kupata mkopo wa matrekta kwa ajili ya
shughuli zao. Tukio hilo lilifanyika jana kwenye Hoteli ya Golden Tulip
jijini Dar es Salaam.Mkuu
wa Kitengo cha Wateja Wakubwa wa Benki ya NMB, Filbert Mponzi (kushoto)
akisaini hati ya makubaliano na Kampuni ya John Deere (wauzaji wa
matrekta) itakayo wawezesha wakulima kupata mkopo wa matrekta kwa ajili
ya shughuli zao. Kutoka kulia ni Mkurugenzi wa Kampuni ya John Deere,
nchi za Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara, Antois van der Westhuizen na
Mkurugenzi Mtendaji wa Lonagro Tatnzania Ltd, Lukas Botha wakishuhudia.Mkurugenzi
wa Kampuni ya John Deere, nchi za Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara,
Antois van der Westhuizen (kulia) akisaini hati ya makubaliano na Benki
ya NMB itakayo wawezesha wakulima kupata mkopo wa matrekta kwa ajili ya
shughuli zao. Kutoka kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Wateja Wakubwa wa
Benki ya NMB, Filbert Mponzi na Mkurugenzi Mtendaji wa Lonagro Tatnzania
Ltd, Lukas Botha, tukio hilo lilifanyika jana kwenye Hoteli ya Golden
Tulip jijini Dar es Salaam.
Na Mwandishi Wetu BENKI ya NMB kwa kushirikiana na Kampuni maarufu kwa
uuzaji wa matrekta ya John Deere zimeingia makubaliano ili kufanikisha
kuwakopesha matrekta wakulia wanaochipuki kwa lengo la kuwawezesha
waendelee kufanya vizuri kwenye kilimo cha kisasa.
Katika makubaliano hayo yaliyofanyika jijini Dar es Salaam Banki ya
NMB imekubali kutoa mkopo ambao utamuwezesha mkulima kununua trekta hilo
huku akiurejesha taratibu, Hata hivyo Kampuni ya John Deere itatoa
mafunzo ya kilimo cha biashara kwa mkulima aliyenufaika na mkopo huo
pamoja na kumfundisha matumizi bora ya kifaa hicho cha kilimo.
Akizungumza mara baada ya kutiliana saini ya makubaliano hayo, Mkuu
wa Kitengo cha Wateja Wakubwa wa Benki ya NMB, Filbert Mponzi alisema
benki yao inatambua umuhimu wa sekta ya kilimo na inavyochangia kukuza
uchumi wa Tanzania hivyo kuamua kuwawezesha wakulima ili kuchochea
ukuaji wa uchumi kwa ujumla.
“…Upatikanaji wa mikopo kwa wakulima siku za nyuma ulikuwa ni kikwazo
kikubwa katika maendeleo ya kilimo…hivyo makubaliano haya yanakuja
kuleta suluhisho kwa wakulima hasa katika eneo la kupata vifaa muhimu
vya kilimo cha kisasa kama matrekta yanayoendana na mabadiliko ya
teknolojia,” alisema Mponzi.
Alisema kwa kutambua mchango wa sekta ya kilimo tayari Benki ya NMB
imewasaidia wakulima wadogo zaini ya 600,000 kupata mitaji ya mikopo kwa
ajili ya uzalishaji wa mazao anuai ya kilimo pamoja na kuendesha
mafunzo ya kijasiliamali kuwajengea uwezo makundi yote.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Kampuni ya John Deere, nchi za Afrika
Kusini mwa Jangwa la Sahara, Antois van der Westhuizen alisema mikopo
hiyo inayotolewa kwa wakulima inalengo la kuwainua wakulima wadogo ili
waweze kubadili kilimo chao kuwa kilimo endelevu kinachotumia vifaa vya
kisasa yakiwemo matrekta ya kilimo, kuvunia na kusafirisha mazao kutoka
shambani hadi eneo linalokusudiwa.
“Kwa kutambua umuhimu wa wakulima wadogo katika nchi za Afrika, John
Deere kwa kushirikiana na NMB tunategemea kuweka mifumo itakayowawezesha
wakulima wadogo ili kuleta ufanisi katika shughuli nzima ya kilimo.
Ufanisi katika manunuzi ya pembejeo, uzalishaji na pia matumizi ya
teknolojia za kisasa (mbegu, mbolea na hata vitendea kazi-mashine) na
hata ufanisi katika kutafuta masoko ya mazao yao mojakwa moja,” alisema
Westhuizen.
Post a Comment