PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: TIMU YA AFC YAPATA AJALI SINGIDA.
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
  NA; YOHANA CHANCE. ARUSHA. Timu ya AFC inayoshiriki ligi daraja la pili (SDL) ilipata ajali wiki iliyopita Mkoani wiki Singida ik...
 
NA; YOHANA CHANCE.
ARUSHA.
Timu ya AFC inayoshiriki ligi daraja la pili (SDL) ilipata ajali wiki iliyopita Mkoani wiki Singida ikiwa inaelekea Mkoani Shinyanga kwenye nchezo wa mwendelezo wa ligi hiyo dhidi ya Bulyanhuru.

Katibu msaidizi wa timu hiyo Charles Mwaimu Alisema kuwa ajali hiyo ilitokea maeneo ya Nanga Mkoani Singida hivyo kufanya wachelewe kufika uwanjani.

“tunamshukuru Mungu hakuna mtu hata mmoja aliyeumia japo kuna baadhi yetu walipata maumvu sehemu mbalimbali za miili yao ila mambo mengine yalienda sawa,maana tulitoa taarifa mara baada ya kutokea tatizo hivyo mchezo wetu ulichelewa kuanza” alisema Mwaimu.

Mchezo huo ulihairishwa mara mbili ambapo ulikuwa ucheze jumapili iliyopita ikashindika kutokana na kuwepo kwa Shinyanga Dabi kati ya Mwadui na Standi United.

Pia ulipendekezwa ucheze siku ya jumatatu wiki hii hivyo uongozi wa AFC ulipeleka Maombi TFF Kuomba mchezo upelekwe tena mbele kutokana na kuwepo kwa uchaguzi wa ubunge jimbo la Arusha jumapili iliyopita, hivyo mchezo huo ulichezwa siku ya jumanne.

Katika mchezo huo AFC walipoteza kwa kufungwa Mabao 3-0 hivyo kujikuta wkipoteza michezo yote ya SDL huku mchezo uliopigwa mwishoni mwa wiki walicheza na Madini Fc Katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid na kutoka sare ya bao 1-0.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top