PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: KWA MWENENDO HUU AFC YA ARUSHA HAITAFIKA MBALI KIMICHEZO.
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
NA; YOHANA CHALLE. ARUSHA. Wadau na Mashabiki wasoka jijini Arusha  waeelezwa kusikitishwa na mwenendo wa timu yao ya AFC  kutokan...
NA; YOHANA CHALLE.
ARUSHA.

Wadau na Mashabiki wasoka jijini Arusha  waeelezwa kusikitishwa na mwenendo wa timu yao ya AFC  kutokana na kupoteza michezo yake yote mitatu tangu msimu wa ligi daraja la pili uanze.

Mwishoni mwa timu ya AFC ililala kwa bao 1-0 dhidi ya JKT Rwankoma mchezo uliopigwa katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid, huku mashabiki walioshuhudia mpambano huo wakiwa na huzuni kubwa kutokana na kiwango kibovu kilichoonyeshwa.

Wakizungumza mara baada ya mpambano huo kumalizika ,Mmoja wa mashabiki hao  Edwini Myuka alieleza kuwa  mwenendo mbovu wa timu ya AFC kwanza unasababishwa na wachezaji wenyewe  kutoonyesha ushirikiano kwani wamekuwa wakipata nasafi na kushindwa kuzitumia ipasavyo.

“Kweli soka la Arusha limeendelea kuwa chini pia likisababishwa na uongozi wa chama cha mpira mkoani hapa kushindwa kutoa ushirikiano kwa timu hii ya wakazi wa jiji la Arusha pasipo kuwaonyesha ushirikiano wa aina yeyeote kwani timu imekuwa ikijiendea yenyewe tu ikionekana kukata tamaa.”alieleza Myuka.

Shabiki mwingine Ally Mohamed Ally alisema  kiwango cha timu cha AFC  kimeshuka sana ukilinganisha hapo awali Kutokana na wadau mbalimbali wa soka kushindwa kabisa kuiunga mkono,Kinachotakiwa timu ikae chini iweze kujipanga upya  msimu ujao.

Omary Habiby aliweza kuiandikia timu yake ya JKT Rwamkomna  bao moja na la pekee lililodumu kwa dakika 90 za mchezo baada ya kuachia shuti kali lililokwenda moja kwa moja nyavuni.

Kocha wa timu ya JKT  Rwamkoma Said Ally Mbwana alisema kuwa  Nidhamu ya mchezo imeisaidia timu yake  kuweza kuibuka na ushindi wa kwanza tena ugenini kutokana na wachezaji kuonyesha kujituma zaidi tangu mpira ulipoanza.

Hata hivyo timu ya AFC  Imepoteza michezo yake mitatu  iliyocheza tangu kuanza kwa ligi ikiwemo michezo yake iliyocheza na timu ya Pamba ya jijini Mwanza na kufungwa mabo 2-0 ,vile vile ilifungwa na timu ya Alliance Spors Academy pia ya Mwanza mbao 3-0 .
 

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top