PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: WANARIADHA ARUSHA WAANZA MAANDALIZI YA MBIO ZA NYIKA.
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
NA; YOHANA CHALLE ARUSHA. Chama cha Riadha mkoa wa Arusha (ARAA) ,kimeanza maandalizi ya msimu mpya wa mbio za Nyika (Cross Country...
NA; YOHANA CHALLE
ARUSHA.

Chama cha Riadha mkoa wa Arusha (ARAA) ,kimeanza maandalizi ya msimu mpya wa mbio za Nyika (Cross Country) katika kuwajenga wanariadha kujiwekea nafasi bora ili waweze kuteuliwa kuingia katika timu ya taifa ya mchezo huu.

Katika ufunguzi wa mbio hizo zilizofanyika katika eneo la  Magereza jijini hapa uliwakutanisha wanariadha  12, huku  kati yao mwanamke akijitokeza mmoja, ambao watakabiliwa na michezo mingine mbele kwa ajili ya kujinoa Zaidi.

Mapema January 9 wanariadha watakwenda Mkoani Kilimanjaro kwa ajili ya mashindano mengine yatakayofikia tamati ifikapo  March 12, 2016 ndipo wanariadha hao watakuwa tayari wamejiongezea Pointi.

Katika mbio hizo wanawake na wanaume waliweza  kukimbia  km 10 na  Panuel Mkungo kutoka klabu ya  holili – Moshi  aliweza kushika nafasi ya kwanza baada ya  kutumia muda wa dakika 31 :24:16,nafasi ya  pili ilikwenda kwa Faraja Lazaro kutoka  pia klabu ya Holili -Moshi aliyetumia muda wa  dakika 32:37:82  na Yohana Elisante  kutoka  Arusha alishika nafsi  ya tatu baada ya kutumia  muda wa  dakika  33:37:88.

Kwa wanawake ilikuwa ni km 8 lakini Bertha  Marco ndiye mwanamke ekee aliyeshiriki na alifanikiwa kutumia muda wa dakika 32:14:90.

Mratibu wa mbio hizo Francis John alieleza kuwa wameanza kuwaweka vijana wawe katika uwezo mzuri kwa ajili ya baadae ili waweze kuteuliwa kuingia timu ya taifa itakayo shiriki  mashindano ya mbio za nyika ya dunia yatakayofanyika  jijini Kampala nchini Uganda ifikapo mwaka 2017.

“Tumeanza msimu mpya wa mbio hizi ambapo wanariadha kutoka mikoa miwili ya Arusha na Kilimanjaro ndio wameweza kujitokeza na kushiriki licha baadhi ya vilabu vya riadha hasa vya majeshi kushindwa kujitokeza kutokana na kuwa  kazi  ulinzi  kwa mujibu wa taarifa tuliyopata” alisema John.

Mbio hizo zimeandaliwa na  kamati ndogo ya mbio za Nyika (Cross Country) huku mbio za barabarani zinatarajia kufanyika kwa msaada wa chama cha  riadha Taifa (RT).

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top