PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: WAGOMBEA HANANG WADAI KUTOKUWA NA IMANI NA MSIMAMIZI WA UCHAGUZI
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
Mgombea Ubunge Jimbo la Hanang Derick Magoma akizungumza na waandishi wa Habari (hawapo pichani) juu ya kutokua na imani na Msimamizi wa ...
Mgombea Ubunge Jimbo la Hanang Derick Magoma akizungumza na waandishi wa Habari (hawapo pichani) juu ya kutokua na imani na Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo hilo ambaye ni Mkurugenzi wa Wilaya ya Hanang Felix Mabula madai ambayo wamewasilisha kwa tume ya uchaguzi iteue Msimamizi ili kufanikisha uchaguzi huru na wa haki.Kushoto ni Mwenyekiti wa Chadema Hanan`g  Isack Joseph  na kulia ni Mgombea udiwani kata ya Endasiwold John Farayo   Picha na Ferdinand Shayo,
 


Na Ferdinand Shayo,Hanang

Wagombea wa Nafasi za Ubunge na Udiwani katika Wilaya ya Hanang iliyoko mkoa wa Manyara wamedai kutokua na imani na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Hanang , Felix Mabula ambaye ni Msimamizi mkuu wa uchaguzi katika jimbo hilo kwa madai kuwa Mkurugenzi huyo alikumbwa na tuhuma nyingi za matumizi mabaya ya fedha kwenye miradi ya maji na kuboresha miundombinu ya shule za msingi tuhuma ambazo ziliibuliwa na madiwani wa CHADEMA  ambao ni wagombea kwa sasa jambo linalowapa wasiwasi kuwa haki haitatendeka katika uchaguzi.

Mgombea Ubunge katika jimbo la Hanang Derick Magoma alisema hayo wakati akizungumza na Waandishi wa Habari ,amesema kuwa tayari wameandikia barua tume ya Uchaguzi yenye kumbukumbu namba CDM/HAN/UT/2/239  juu ya kutokua na imani na msimamizi wa Uchaguzi wa jimbo hilo barua waliyoiwasilisha septemba 2 mwaka huu wakiitaka tume iteue Msimamizi mwingine.

Magoma alisema kuwa tuhuma za matumizi mabaya ya fedha zilijadiliwa katika Baraza la Madiwani zikiongozwa na madiwani wa CHADEMA ambao ni Ndugu Peter Lori Diwani wa Kata ya Katesh,John Farayo Diwani kata ya Endasiwold ,Masala Bajuta wa kata ya Gisambalang na wengine wengi.

“Madiwani hao waliomtuhumu Mabula  ndio wagombea    na hao hao Mabula atasimamia uchaguzi wao ,tunaona kabisa kuwa haki haiwezi kutendeka ,na hata kama ikitendeka hatutaamini kama imetendeka” Alisema Magoma

Mgombea huyo alisema kuwa Mabula anakabiliwa na tuhuma za kutumia vibaya shilingi bilioni 1 na milioni 100 ambazo zimepotea na zingetumika kujenga vituo vya afya ,kuleta madawa na kusambaza huduma ya maji safi ambayo ni changamoto kubwa kwa jimbo hilo.

Mgombea udiwani kata ya Endasiwold John Farayo alisema kuwa wao kama wagombea hawana imani na Mkurugenzi huyo hivyo wameitaka tume ya uchaguzi ichukue hatua za haraka kumteua msimamizi mwingine wa uchaguzi ili uchaguzi uwe huru na wa haki.

Mwenyekiti wa Chadema Hanan`g  Isack Joseph alisema kuwa chama hicho kimesimamisha wagombea  udiwani 31 kati ya kata 33 na kufafanua kuwa kutokana na rekodi ya Mkurugenzi huyo wanahitaji msimamizi mwingine wa uchaguzi ambaye watakua na imani naye.





About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top