PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: PANONE FC KUENDELEZA UBABE FDL.
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
NA; YOHANA CHALLE. MOSHI. Timu ya  Panone  FC ya mjini Moshi, mkoani Kilimanjaro maarufu kama matajiri wa mafuta ,inaahidi kuendele...

NA; YOHANA CHALLE.
MOSHI.

Timu ya Panone FC ya mjini Moshi, mkoani Kilimanjaro maarufu kama matajiri wa mafuta ,inaahidi kuendeleza kichapo kwa kila timu inayokutana nayo katika ligi daraja la kwanza iliyoanza kutimua vumbi mwishoni mwa wiki.

Panone katika mchezo wake wa kwanza uliochezwa katika uwanja wa ushirika mjini mshi dhidi ya JKT Oljoro waliibuka na ushindi wa bao 4-0 na kuweka matumaini ya kufanya vizuri zaidi katika ligi hiyo.

Msemaji wa timu hiyo Husein Mwinyi alisema kuwa kwa sasa timu hiyo wanajiandaa kuchukua alama tatu nyingine mwishoni mwa wiki watakapoikaribisha timu ya Polis Tabora

“Licha ya kupata ushindi katika mchezo uliopita dhidi ya JKT Oljoro bado kocha hajalidhika na wachezaji wake kutofuata maelezo hasa katika eneo la katikati wachezaji walikuwa hawaelewani vizuri” alisema Mwinyi.

Mara baada ya mchezo wa mwishoni mwa wiki dhidi ya Polis Tabora, Panone FC itaelekea mjini Kigoma kupambana na JKT kanembwa.

Hadi sasa Pnone ndio wanaoongoza kundi C kwa kujikusanyia alama tatu na mabao 4, huku Polis Tabora wakifuatia wakiwa na alama tatu na mabao matatu.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top