PRINCE MEDIA TZ PRINCE MEDIA TZ Author
Title: JKT OLJORO YAJIPANGA KIVINGINE.
Author: PRINCE MEDIA TZ
Rating 5 of 5 Des:
NA, YOHANA CHALLE. ARUSHA. Mara baada ya kupokea kichapo cha mabao 4-0 mwishoni mwa wiki dhidi ya Panone, Oljoro inajiandaa kueleke...
NA, YOHANA CHALLE.
ARUSHA.

Mara baada ya kupokea kichapo cha mabao 4-0 mwishoni mwa wiki dhidi ya Panone, Oljoro inajiandaa kuelekea Tabora mwishoni mwa wiki kucheza na Rhino Rangers katika mwendelezo wa ligi daraja la kwanza.

Katibu mkuu wa Oljoro Husein Nalinga alisema kuwa wachezaji wa timu hiyo wanaendelea na mazoezi katika uwanja wa general Tyre njiro kulingana na ratiba ya kocha.

“kocha mkuu wa timu bado ni mgeni hana hata mwezi na bado hajawazoea wachezaji vizuri, lakini anawahaidi wapenzi na mashabiki wa Oljoro kulekebisha makosa yaliyojitokeza katika mchezo uliopita dhidi ya Panone” alisema Nalinga.

JKT Olojro ipo katika kundi ‘C’ pamoja na timu za Panone ,Polisi Mara –Mara,Rhino Rangers –Tabora,Mbao fc –Mwanza,Polisi Tabora  -Tabora,Geita Gold –Geita na JKT  Kanembwa – kigoma.

Timu hiyo ndio tegemeo kwa wakazi wa Arusha ili kuhakikisha wanapata timu itakayoshiriki ligi kuu Tanzania Bara msimu ujao, kwani tangu AFC inayoshiriki ligi daraja la Pili na Oljoro zishuke daraja wakazi wa Mkoa huu hawajashuhudia timu yoyote kubwa ilikuja kucheza mchezo hata wa kirafiki.

Nalinga aliongeza kuwa licha ya kupoteza mchezo wa kwanza bado timu hiyo inweza kurudi ligi kuu kwa kuwa ligi bado mbichi na watajipanga na kufanya vizuri zaidi.

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top