Na Ferdinand Shayo,Arusha.
Serikali imetwaa jumla ya Ekari 7000 baada ya ubatilishwaji
wa Mashamba ya Tanzania plantatition limited yaliyokua yakimilikiwa na
mwekezaji kutoka nje ,mashamba hayo
yanatajiwa kugawanywa kwa wananchi 2000 wenye uhitaji wa ardhi ya makazi na
mashamba .
Aidha baada ya ubatilishwaji wa mashamba hayo Arusha imepata
ekari 6176.5 na Halmashauri ya Meru ekari 925
hivyo kufikia ekari 7101 ambazo zitagawanywa kwa wananchi.
Hayo yameelezwa na Waziri wa Ardhi Nyumba na Makazi,Wiliam
Lukuvi wakati akitoa taarifa ya usuluhishi wa migogoro ya ardhi katika mikoa ya Arusha na Manyara katika
mkutano wake na Waandishi wa Habari,Lukuvi amesema kuwa mashamba hayo yalikua
na migogoro kwa kipindi kirefu kati ya mwekezaji na Wananchi hivyo kutokana na
uhitaji mkubwa wa ardhi serikali imeamua kubatilisha mashamba hayo.
“Nimekuja Arusha na timu yangu ambayo itafanya uhakikiki wa
watu 2000 wenye uhitaji na baada ya kujiridhisha watafanya zoezi la ugawaji na
pia wananchi watapatiwa hati ya kumiliki ardhi zao safari hii hatutagawa ardhi
kienyegi” Alisema Lukuvi
Lukuvi amesema kuwa mbali na shamba hilo pia wamepata ekari
100 katika shamba la Imani Estate na pia Shamba la Noors lenye Ekari 2296 lililokua na mgogoro kati ya Mwekezaji na
wananchi wa Kijiji cha Laroi na Kisima cha Mungu litagaiwa kwa wananchi baada
ya mazungumzo kati ya Mwekezaji kukubali kuachia shamba hilo
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Arusha DC ,Fidelis Lumato
amesema kuwa ugawanywaji wa mashamba hayo utasaidia kupunguza migogoro mikubwa
ya ardhi iliyokua inakabili wilaya hiyo kutokana na uhaba mkubwa wa ardhi.
Jumla ya migogoro 80
iliyowasilishwa kwa Waziri Lukuvi kutoka katika Halmashauri ya Jiji la Arusha ,Halmashauri
ya Wilaya ya Arusha na Halmashauri ya Meru imepatiwa ufumbuzi hivyo kupunguza
migogoro ya ardhi ilikua ikilisakama jiji la Arusha.
Post a Comment